Saturday, November 10, 2012

TAZAMA MASHABIKI WA SIMBA TANGA WALIVYOIPIGA KIBERITI JEZI YA YANGA LEO KWENYE UWANJA WA MKWAKWANI... NI SIKU MOJA TU BAADA YA MASHABIKI WENGINE TANGA KULIPIGA MAWE BASI LA YANGA WAKATI LIKIPITA ENEO LA KABUKU NA KUPASUA KIOO!

Mashabiki wanaodhaniwa kuwa ni wa Simba wakionekana kufurahia baada ya kuitia kiberiti jezi ya Yanga inbayoonekana ikiteketea kwa moto wakati wa mechi ya raundi ya 13 ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara kati ya Mgambo JKT na Azam FC kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga leo Novemba 10, 2012.
Basi la Yanga
Siku moja tu baada ya basi la Yanga kupigwa mawe na mashabiki wa soka wanaodhaniwa kuwa ni wa klabu ya Simba wakati likipita kwenye eneo la kitongoji cha Kabuku mkoani Tanga na kupasua kioo cha gari, tukio jingine la hatari limefanywa leo na mashabiki wanaodhaniwa pia kuwa ni wa 'Wekundu wa Msimbazi' jijini Tanga baada ya kuitia kiberiti hadharani jezi ya watani zao wa jadi huku wakishangilia na kupiga makofi.

Tukio hilo limetokea kwenye jukwaa la kusini mwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wakati wa mechi ya Ligi Kuu ya Bara kati ya wenyeji JKT Mgambo na Azam ambapo shabiki mmoja aliyevalia jezi ya Yanga, alivuliwa wakati wa mapumziko na kisha jezi hiyo ikachomwa moto huku wengine wakishangilia na kupiga makofi.


Mbaya zaidi, mashabiki hao waliokuwa akifurahia kitendo hicho hawakuonekana kufanya jiotihada zozote za kumvisha mtu waliyemvbua jezi hiyo ambaye kwa dakika kadhaa alionekana akiwa tumbo wazi na kujawa na fadhaa kubwa huku wapinzani wake wakimcheka na kuapiza kuwa piga ua, lazima 'Wanajangwani'  watachezea kichapo kesho  katika mechi yao ya mwisho ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Bara dhidi ya wenyeji Coastal Union.

Juzi, basi la Yanga lilipigwa mawe na watu wanaodhaniwa kuwa ni mashabiki wa Simba na kioo kimojawapo kikapasuka na inasemekena kuwa straika Simkon Msuva wa vinara hao wa ligi kuu ya Bara alipata jeraha.

Yanga watashuka dimbani kwenye Uwanja wa Mkwakwani kesho huku wakijua kwamba matokeo yoyote watakayopata hayatawaathiri kwenye msimamo wa ligi kwani hadi sasa wanaongoza kwa kuwa na pointi 26 baada ya kucheza mechi 12, pointi mbili zaidi ya Azam waliopokea kipigo kisichotarajiwa cha mabao 2-1 kutoka kwa Azam na pointi tatu zaidi ya mahasimu wao wa jadi, Simba waliochezea kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Toto African ya Mwanza.

1 comment: