Sunday, June 16, 2013

RONALDO AMWAMBIA BALOTELLI: USIUE KIPAJI CHAKO KAMA ADRIANO

Ronaldo de Lima akiwa matembezi na rafikiye wa kike, DJ Paula Morais
Ronaldo de Lima akiwa matembezi na rafikiye wa kike, DJ Paula Morais
Ronaldo de Lima akifanya shopping na rafikiye wa kike, DJ Paula Morais, mjini Madrid, Hispania
Balotelli akiwa matembezi na rafikiye wa kike
Mario Balotelli akijifua na wenzake wa timu ya taifa ya Italia katika maandalizi ya kushiriki Kombe la Mabara kwenye Uwanja wa Estadio Joao Havelange mjini Rio de Janeiro, Brazil.

Mario Balotelli akijifua na wenzake wa timu ya taifa ya Italia katika maandalizi ya kushiriki Kombe la Mabara kwenye Uwanja wa Estadio Joao Havelange mjini Rio de Janeiro, Brazil.

Mario Balotelli akijifua na wenzake wa timu ya taifa ya Italia katika maandalizi ya kushiriki Kombe la Mabara kwenye Uwanja wa Estadio Joao Havelange mjini Rio de Janeiro, Brazil.

Mario Balotelli akijifua na wenzake wa timu ya taifa ya Italia katika maandalizi ya kushiriki Kombe la Mabara kwenye Uwanja wa Estadio Joao Havelange mjini Rio de Janeiro, Brazil.


RONALDO de Lima amemshauri mshambuliaji wa AC Milan, Mario Balotelli, asiache kipaji chake kipotee kama nyota wa zamani wa Inter Milan na Brazil, Adriano.

Aliliambia Gazzetta dello Sport: “Balotelli amejaliwa kipaji kikubwa, anajua namna ya kuufanya mpira katika hali fulani na kuutumbukiza wavuni.

"Lakini hapaswi kuridhika na alipofikia na hapaswi kutumia umri wake kama kisingizio cha kufanya vitu vya kipuuzi uwanjani.

“Kama straika anajua kucheza, lazima wapinzani watamchokoza kwa kumchapa viatu. Nafahamu vyema hili, kama ningekuwa narudishia kila anayenipiga kiatu... sote tunafanya mambo ya kijinga maishani mwetu, lakini ni lazima tubaini kwamba ni wakati wa kuacha. Hesabu hadi tano kabla ya kujibu.

"Ananikumbusha Adriano, ingawa suala lao ni tofauti. Adriano alikuwa na ufundi na nguvu, hivyo angefanya chochote uwanjani, lakini kulikuwa na wakati uzalendo unamshinda."

"Ushauri wangu kwa Balotelli ni huu: usipoteze kipaji chako. Kwenye Uwanja wa Maracana unaweza kujua nani mchezaji wa kweli na nani anafulia, hivyo namwambia asipagawishwe na hali hiyo. Kucheza pale kunakupa mizuka, kwa sababu ni moja ya viwanja bora zaidi duniani. Sikuwahi kufunga goli la kimashindano katika uwanja wa Maracana."

No comments:

Post a Comment