Tuesday, March 26, 2013

TAZAMA A-Z YA NAMNA WEMA SEPETU AlLIVYOMUOKOA KAJALA ASIENDE LUPANGO KUTUMIKIA KIFUNGO CHA MIAKA SABA JELA… NI BAADA YA KUMLIPIA CHAP- CHAP FAINI YA SHILINGI MILIONI 13… HATA HIVYO MUME WA KAJALA AKOSA WA KUMLIPIA FAINI YA SH. MIL. 213 NA KUTUPWA JELA MIAKA 12

Pole shosti... ndiyo mipango ya Mungu! Wema (kulia) akimfariji Kajala.
Imeniuma sana... shosti 'ngu Kajala hawezi kwenda jela... Lazima nikadroo mkwanja wangu benki nimtoe leo leo! Wema akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kuchangamkia dili la kumchomoa Kajala kwa kumlipia faini ya mil.13 fastaaaa....!

Haa haa haaaa haaaa... Wema akifurahia na Kajala baada ya kufanikiwa kumchomoa lupango kwa kulipa mkwanja alioamuru pilato wa 'em 13' taslim! Chezea Wema weye!

Siamini uko huru shosti ... jela ni nomaaaa! Msanii Elizabeth Michael a.k.a Lulu akibubujikwa machozi baada ya shost yake Kajala kuachiwa huru. Lulu naye aliachiwa kwa dhamana hivi karibuni kutokana na kesi inayomkabili ya kudaiwa kumuua Kanumba bila kukusudia.

Kicheko cha furaha...


Pole sana mamaa... Msanii Dk. Cheni akimfariji Kajala

Mama yake Lulu aitwaye Lucrecia Karugila (kushoto) akiongoza kikao kidoooogo nje ya mahakama ya Kisutu kuhusiana na namna ya kumchomoa Kajala

Dah... yaani mamwela swalishamswaga Kajala kwenye karandinga kuanza safari kwenda lupango. Wema alicheza kama Pele kwenda kuwahi kulipa faini na kumuokoa asiende jela...!

Tutamtoaje? Lulu na shosti yake mmoja wakijadili namna ya kumchomoa Kajala

Hapa ni wakati akipelekwa kwa pilato kusomewa hukumu

Akielekea kwenye karandinga kabla ya Wema kumchomoa

Sijui itakuwaje? Hapa ni kabla Wema hajafanya makaratee yake na kumchomoa... karandinga lilishakuwa tayari kumbeba na kumpeleka lupango chini ya ulinzi mkali wa 'mamwela' wa Magereza
Msanii nyota wa filamu, Kajala Masanja alihukumiwa kwenda jela kutumikia kifungo cha miaka saba au kulipa faini ya fedha taslim Sh. milioni 13 baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisuti jijini Dar es Salaam kumkuta na hatia ya makosa mawili ya kula njama na kuuza nyumba iliyokuwa chini ya uchunguzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Mume wa Kajala aitwaye Faraja Chambo, pia alikumbana na adhabu ya kifungo cha kwenda jela miaka 12 au kulipa faini ya Sh. milioni 213 baada ya kukutwa na hatia kutokana na makosa hayo na jingine la tatu la utakatishaji fedha.

Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Sundi Fimbo wa Mahakama ya Kisutu.
Hata hivyo, wakati mumewe Chambo akipelekwa gerezani baada ya kushindwa sharti la kulipa faini, Kajala aliachiwa huru saa chache baadaye kufuatia msanii mwenzake nyota wa filamu nchini, Wema Sepetu kuwahi kwenda benki na kurejea mahakamani kumlipia faini (Sh. milioni 13).

Mwishowe, baada ya kukamilisha taratibu zote mahakamani hapo, Kajala akaachiwa huru saa 7:37 mchana na kulakiwa na ndugu, jamaa na marafiki waliojazana tele kujua hatma yake; baadhi yao wakiwa ni wasanii Elizabeth Michael Michael 'Lulu', Muhsen Awadh "Dk. Cheni' . Miongoni mwao alikuwapo pia mama yake Lulu, Lucresia Karugila.

KESI YENYEWE
Awali, wakati Hakimu Fimbo akisoma hukumu ya kesi hiyo kuanzia saa 4:33 hadi saa 5:49 asuhuhi, Kajala alionekana kizimbani akibubujikwa machozi muda wote.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Fimbo alisema baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na pande zote mbili, mahakama imewatia hatiani washtakiwa wote wawili kwa makosa mawili ambayo ni pamoja na kula njama ya kuhamisha umiliki wa nyumba iliyopo Kunduchi Salasala jijini Dar es Salaam.

Washtakiwa hao, pia kwa pamoja walikutwa na hatia ya shtaka la pili la kuhamisha isivyo halali umiliki wa nyumba hiyo kwenda kwa Emiliana Rwegarura huku wakijua kwamba imepatikana kwa  njia ya rushwa.

"Siuo kweli kama washtakiwa hawakujua kuwa kuna hati ya kuzuia nyumba hiyo kuuzwa... lakini waliidharau hati hiyo na kuiuza nyumba hiyo kinyume cha sheria," alisema Hakimu Fimbo.

"Mshtakiwa wa kwanza (mume wa Kajala) amekutwa na hatia pia katika shtaka la tatu kwa sababu ushahidi umeonyesha kuwa alizipata fedha hizo kwa njia ya utakatishaji haramu na Kajala ameachiwa huru kwavile hakujua fedha hizo zilipatikana vipi... lakini alihusika katika kuuza nyumba hiyo," alisema Hakimu Fimbo.

Kabla ya kusomwa adhabu ya washtakiwa hao, Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Leonard Swai, aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa washtakiwa ili iwe fundisho kwa watu wenye tabia kama ya washtakiwa.

Katika kesi hiyo, washtakiwa walikuwa wanakabiliwa na mashtaka matatu, likiwamo  la kuhamisha umiliki, kula njama kinyume cha kifungu cha 34 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007 huku wakijua ni kosa kwani tayari Mwanasheria Mkuu wa serikali alishazuia uuzwaji wa nyumba hiyo.

Katika shtaka la pili, ilidaiwa kuwa Aprili 14 mwaka 2010, washtakiwa hao walihamisha isivyo halali umiliki wa nyumba hiyo kwenda kwa Emiliana Rwegarura huku wakijua imepatikana kwa njia ya rushwa, kinyume cha kifungu cha 34(2)A(3) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007.

Katika shtaka la tatu, ilidaiwa kuwa siku na mahali hapo washitakiwa hao walitakatisha fedha huku wakijiua ni kinyume na sheria hiyo.

Awali, kwa nyakati tofauti, washtakiwa walikana mashtaka yote lakini kwavile mashtaka hayo hayana dhamana kisheria, wote wawili walikuwa mahabusu hadi jana ilipotolewa hukumu.

No comments:

Post a Comment