Tuesday, February 12, 2013

PATA MAJINA 14 YA VIGOGO WA CCM WALIOPITISHWA KUWA WAJUMBE WA KAMATI KUU CCM (CC) .... WAMO 'DOGO' JERRY SLAA, STEPHEN WASSIRA 'TYSON', DOKTA HUSSEIN MWINYI, DOKTA EMMANUEL NCHIMBI NA PROFESSA ANNA TIBAIJUKA... WANAOTAJWA URAIS KAMA EDWARD LOWASSA, SAMWEL SITTA NA MEMBE WATOSWA!

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete
Hatimaye kikao cha Halmashayri Kuu ya CCM (NEC) kilichoketi kwa siku mbili mjini Dodoma (Februari 10 na 11, 2013) kimepitisha majina 14 ya wajumbe wa Kamati Kuu (CC) ya chama hicho ambapo kinyume na matarajio ya wengi, vigogo kadhaa wamejikuta wakitoswa na badala yake kuingizwa kwa damu kadhaa mpya katika siasa za chama hicho tawala, akiwamo Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Slaa.

Vigogo wanaotajwatajwa kuwa wana 'usongo' wa kuwania urais mwaka 2015 kama waziri mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, Waziri wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta na Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa, Bernad Membe, wameachwa ndani ya chombo hicho cha juu zaidi, ambacho huwa kina wajumbe saba kutoka Bara na wengine wa idadi hiyo kutoka Zanzibar.

Kwa kawaida, majina ya wajumbe hao hupendekezwa na mwenyekiti wa chama na hivyo, Rais Jakaya Kikwete ndiye aliyewateua na wajumbe wa NEC kuwapitisha.

Majina ya wajumbe saba wa kamati kuu  (CC) ya CCM waliopitishwa kutoka Bara ni:
1. Pindi Chana
2. Adam Kimbisa
3. William Lukuvi
4. Dk. Emmanuel Nchimbi
5. Jerry Slaa
6. Prof. Anna Tibaijuka
7. Stephen Wassira

Kutoka Zanzibar, wajumbe saba waliopitishwa katika CC ya CCM ni:
1. Shamsi Vuai Nahodha
2. Dk. Hussein Mwinyi
3. Prof. Makame Mbarawa Mnyaa
4. Dk. Salim Ahmed Salim
5. Dk. Maua Daftari
6. Samia Suluhu Hassan
7. Hadija H. Aboud

Kwa utaratibu wa CCM, wajumbe wa CC ndiyo wenye rungu la kuchuja majina ya wagombea wote wa urais kupitia chama hicho ambapo mwishowe hupeleka majina ya mwisho ya wale wote wenye sifa kwenye mkutano wa halmashauri kuu (NEC) ili hatimaye kubaki na mgombea mmoja anayepeperusha bendera ya chama hicho wakati wa uchaguzi mkuu.

Hivyo, ni wajumbe hawa 14 ndiyo watakaoamua hatma ya wagombea urais wa CCM, kwani wanao uwezo wa kufyeka jina la mgombea yeyote kwa sababu watakazoona kuwa zinafaa wakati wa mchakato wa uchaguzi mkuu wa 2015 utakapoanza kwa kusaka wagombea ndani ya vyama, kikiwamo CCM.

No comments:

Post a Comment