Monday, January 28, 2013

LULU ABUBUJIKWA MACHOZI YA FURAHA KORTINI... NI BAADA YA JAJI KUMPA MASHARTI AMBAYO AKIYATIMIZA ATAACHIWA KESHO MARA MOJA NA KUACHANA NA MAUGALI YALIYOMNENEPESHA JELA NA KWENDA KULA UBWABWA SAAAAAAAFI WA NYUMBANI KWAOOOOO....!

Elizabeth Michael a.k.a Lulu akitoka mahakamani leo kuelekea kupanda karandinga



Mwanionaje? Nimenenepa eenh! Lulu akitoka mahakamani kwenda kupanda "karandinga" leo




Msanii  wa filamu Elizabeth Michael 'Lulu' amejikuta akibubujikwa machozi ya furaha leo baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kumpa masharti ya dhamana ambayo akiyatimiza ataachana na maisha ya rumande kuanzia kesho.

Lulu amekuwa rumande kwa takriban mwaka mmoja sasa kuhusiana na shitaka la kumuua bila kukusudia aliyekuwa msanii mwenzake wa filamu, marehemu Steven Kanumba.

“Naomba Mungu anisaidie nipate dhamana na kurudi nyumbani,” Lulu alisema leo huku akilia kwa furaha katika viunga vya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.

Jaji Zainabu Mruke ndiye aliyetoa masharti hayo  jana baada ya wakili wa utetezi, Peter Kibatala kuwasilisha maombi ya dhamana kwa hati ya dharura chini ya kifungu cha 148 kidogo cha (1) na cha (2) cha Mwenendo wa Sheria ya Makosa ya Jinai (CPA).
Upande wa Jamhuri uliongozwa na wakili wa serikali, Joseph Maugo na Kishenyi Mutalemwa.

Jaji Mruke alisema kosa linalomkabili mshitakiwa lina dhamana kisheria na kwamba mshtakiwa atakuwa nje kwa dhamana kwa kufuata masharti ya kuwa na wadhamini wawili ambao ni watumishi wa serikali watakaosaini hati ya dhamana ya Sh. milioni 20 kila mmoja.


Pia amemtaka Lulu atimize sharti la kuwasilisha hati zake za kusafiria, kuripoti kila tarehe mosi ya mwezi kwa Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na asitoke nje ya mkoa wa Dar es Salaam bila kibali cha msajili huyo.
Akitimiza masharti hayo kesho, Lulu ataachiwa kwa dhamana na kurejea nyumbani kwao.

Katika kesi ya msingi, Lulu anadaiwa kuwa  Aprili 7, 2012, katika eneo la Sinza Vatican jijini Dar es Salaam, alimuua Kanumba bila kukusudia.

No comments:

Post a Comment