Sunday, December 30, 2012

LAMPARD APIGA 2 KUIPAISHA CHELSEA HADI NAFASI YA TATU KATIKA MSIMAMO WA LIGI KUU YA ENGLAND... NI BAADA YA USHINDI WA 2-1 DHIDI YA EVERTON... SASA YABAKIZA POINTI 4 KUIKAMATA MAN CITY HUKU IKIWA NA MECHI MOJA MKONONI


Frank Lampard wa Chelsea (katikati) akishangilia baada ya mechi kumalizika huku akiwa amefunga magoli yote mawili wakati Chelsea ikishinda 2-1 dhidi ya Everton katika mechi yao ya Ligi Kuu ya England kwenye Uwanja wa Goodison Park mjini Liverpool, leo Desemba 30, 2012. (Picha: REUTERS)
Natishaaa....! Lampard akiwapungia 'dole' mashabiki baada ya mechi yao dhidi ya Everton kumalizika leo Desemba 30, 2012.

Chelsea Frank Lampard (kushoto) akishangilia goli alilofunga na mwenzake Juan Mata wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya England kwehnye Uwanja wa Goodison Park mjini Liverpool, leo Desemba 30, 2012. Chelsea imeshinda 2-1. (Picha:  REUTERS)
Steven Pienaar wa Everton (kushoto) akichuana na David Luiz wa  Chelsea wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya England kwenye Uwanja wa Goodison Park mjini Liverpool, jana. (Picha: REUTERS)


LONDON, England
FRANK Lampard alionyesha thamani yake kwa  Chelsea baada ya kufunga magoli mawili ‘makali’ yaliyoipa ushindi wa ugenini wa mabao 2-1 dhidi ya Everton leo na kukwea hadi katika nafasi yake ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England. 

Huku kukiwa na uvumi mwingi kuhusiana na hatma yake ndani ya Chelsea, alionyesha kiwango cha juu na kufunga mabao yote huku goli la Everton likifungwa na Steven Pienaar. 

Ushindi wan ne mfululizo wa Chelsea chini ya kocha Rafael Benitez umeiinua hadi kubakiza pointi nne tu kabla ya kuifikia Manchester City inayoshika nafasi ya pili, huku Chelsea ikiwa na mechi moja mkononi.

No comments:

Post a Comment