Thursday, December 20, 2012

CHELSEA YAWASAMBARATISHA KINA EL HADJI DIOUF 5-1, YATINGA NUSU FAINALI CAPITAL ONE CUP... SASA KUWAVAA SWANSEA

Fernando Torres (kushoto) wa Chelsea akipongezwa na mchezaji mwenzake Frank Lampard baada ya kuifungia timu yake goli la tano wakati wa mechi yao ya robo fainali ya Kombe la Ligi (Capital One Cup) dhidi ya Leeds United kwenye Uwanja wa Elland Road mjini Leeds, England jana usiku Desemba 19, 2012. Chelsea ilishinda 5-1.
Victor Moses wa Chelsea akishangilia kuifungia timu yake goli la tatu wakati wa mechi yao ya robo fainali ya Kombe la Ligi (Capital One Cup) dhidi ya Leeds United kwenye Uwanja wa Elland Road mjini Leeds, England jana usiku Desemba 19, 2012. Chelsea ilishinda 5-1.
 
Victor Moses wa Chelsea akishangilia kuifungia timu yake goli la tatu wakati wa mechi yao ya robo fainali ya Kombe la Ligi (Capital One Cup) dhidi ya Leeds United kwenye Uwanja wa Elland Road mjini Leeds, England jana usiku Desemba 19, 2012. Chelsea ilishinda 5-1.
 
Juan Mata wa Chelsea akishangilia kufunga goli la kwanza la timu yake na kufanya matokeo yawe 1-1 pamoja na mchezaji mwenzake Cesar Azpilicueta (kushoto) wakati wa mechi yao ya robo fainali ya Kombe la Ligi (Capital One Cup) dhidi ya Leeds United kwenye Uwanja wa Elland Road mjini Leeds, England jana usiku Desemba 19, 2012. Chelsea ilishinda 5-1.

Juan Mata wa Chelsea akishangilia kufunga goli la kwanza la timu yake na kufanya matokeo yawe 1-1 pamoja na mchezaji mwenzake Cesar Azpilicueta (kushoto) wakati wa mechi yao ya robo fainali ya Kombe la Ligi (Capital One Cup) dhidi ya Leeds United kwenye Uwanja wa Elland Road mjini Leeds, England jana usiku Desemba 19, 2012. Chelsea ilishinda 5-1.
Luciano Becchio wa Leeds United akishangilia kufunga goli la kuongoza pamoja na mchezai mwenzake El-Hadji Diouf (kulia) wakati wa mechi yao ya robo fainali ya Kombe la Ligi (Capital One Cup) dhidi ya Chelsea kwenye Uwanja wa Elland Road mjini Leeds, England jana usiku Desemba 19, 2012. Chelsea ilishinda 5-1.

Luciano Becchio wa Leeds United akishangilia kufunga goli la kuongoza pamoja na mchezai mwenzake El-Hadji Diouf (kulia) wakati wa mechi yao ya robo fainali ya Kombe la Ligi (Capital One Cup) dhidi ya Chelsea kwenye Uwanja wa Elland Road mjini Leeds, England jana usiku Desemba 19, 2012. Chelsea ilishinda 5-1.
Gooooooooo! Branislav Ivanovic (kulia) wa Chelsea akifunga goli la pili kwa kichwa dhidi ya Leeds jana usiku

CHELSEA walizinduka kutoka nyuma na kuisambaratisha Leeds kwa mabao 5-1 kwenye uwanja wa Elland Road na kutinga nusu fainali ya Kombe la Ligi (Capital One Cup) jana usiku.

Luciano Becchio alimalizia vyema shambulizi la kustukiza na kuwapa wenyeji uongozi wa 1-0 hadi wakati wa mapumziko pamoja na matumaini ya kupata ushindi maarufu.

Lakini Juan Mata alifunga la kusawazisha dakika mbili baada ya kipindi cha pili kuanza na Branislav Ivanovic akafunga kwa kichwa katika dakika 64 kuiweka Chelsea mbele.

Victor Moses akafunga kwa shuti lililotinga kwenye kona ya chini ya lango kufuatia shambulizi la kustukiza katika dakika ya 66 kabla ya Eden Hazard kufunga la nne katika dakika 85 na Fernando Torres akamalizia kiulaini la tano katika dakika 87 na kuipeleka Chelsea katika hatua ya nusu fainali.

Yalikuwa ni matokeo ambayo yalidumisha rekodi yao ya kutofungwa dhidi ya Leeds katika michuano ya kuwania vikombe na kuwarejesha katika mwendo wao wa kushinda baada ya kufungwa na Corinthians katika fainali ya Kombe la Dunia la Klabu.

Kwa ushindi huo, Chelsea itaikabili Swansea katika mechi mbili za nusu fainali zitakazochezwa Januari 7 na marudiano Januari 21. Mechi nyingine ya nusu fainali itakayochezwa tarehe hizo hizo itakuwa ni baina ya Bradford iliyoitoa Arsenal dhidi ya Aston Villa.


Vikosi vilikuwa



Leeds United

  • 12 Ashdown
  • 02 Peltier
  • 04 Lees
  • 05 Pearce
  • 07 Green
  • 09 Thomas (White - 68' )
  • 17 Brown (Norris - 72' )
  • 18 Tonge
  • 25 Byram
  • 10 Becchio
  • 21 El Hadj Diouf (McCormack - 72' )

Wachezaji wa akiba

  • 01 Kenny
  • 11 Varney
  • 14 White
  • 19 Norris
  • 20 Gray
  • 28 Somma
  • 44 McCormack

Chelsea

  • 01 Cech
  • 02 Ivanovic
  • 04 David Luiz
  • 28 Azpilicueta
  • 34 Bertrand (Cole - 74' )
  • 08 Lampard 
  • 10 Mata (Ferreira - 85' )
  • 11 Oscar
  • 13 Moses
  • 21 Marin (Hazard - 60' )
  • 09 Torres

Wachezaji wa akiba

  • 22 Turnbull
  • 03 Cole
  • 19 Ferreira
  • 17 Hazard
  • 56 Saville
  • 57 Ake
  • 35 Piazon


Refa: Marriner

Mashabiki waliohudhuria: 33,816

No comments:

Post a Comment