![]() |
Theo Walcott |
![]() |
Bacary Sagna |
LONDON,
England
KLABU
ya Arsenal imemuacha straika Theo Walcott aliye katika mvutano na timu hiyo
kuhusiana na mkataba wake mpya kwenye kalenda yao ya mwaka 2013, imefahamika.
Gazeti
la The Sun limesema vilevile kuwa Bacary Sagna, ambaye pia anaisumbua klabu
hiyo katika mazungumzo yao kuhusu kusaini mkataba mpya, ni mchezaji mwingine
nyota aliyeachwa katika kalenda rasmi ya timu hiyo kwa mwaka ujao.
Walcott
(23), haonekani kokote katika toleo la kalenda hiyo ya mwakani baada kushindwa
kuwahakikishia kwamba atabaki klabuni hapo.
Straika
huyo wa kimataifa wa England, ambaye hivi sasa anapokea mshahara wa paundi za
England 65,000 kwa wiki katika mkataba utakaomalizika Juni, alikataa ofa
aliyopewa y kusaini mkataba mpya utakaombatana na mshahara wa paundi za England
80,000 kwa wiki.
Mgomo
wake huo tayari umeziamsha klabu kadhaa za Ligi Kuu ya England zikiwamo za
Liverpool na Manchester City, ambao wanaaminika kuwa wako tayari kuilipa
Arsenal paundi za England milioni 15 ili kumnasa wakati wa kipindi cha uhamisho
wa dirisha dogo la Januari.
Kocha
wa Arsenal, Arsene Wenger amesema wazi kwamba anataka na anatarajia kwamba
Walcott atasaini mkataba mpya wa kumbakiza katika klabu yao.
Hata
hivyo, wengi wanaamini kwamba sasa Arsenal wameshakubali kumpoteza Walcott
baada ya litomjumuisha katika kalenda yao mpya ya mwaka 2013, ingawa Wenger amedai
kwamba kuachwa katika kalenda si ishara kwamba nyota hao watapigwa bei.
No comments:
Post a Comment