Tuesday, November 13, 2012

ONA MAPICHA KIBAO YA MBWEMBWE ZA MASHABIKI WA YANGA WAKATI WAKISHINDA 2-0 DHIDI YA COASTAL UNION JIJINI TANGA NA KUJICHIMBIA KILELENI MWA MSIMAMO WA LIGI KWA TOFAUTI YA POINTI TANO YA AZAM INAYOSHIKA NAFASI YA PILI NA SITA DHIDI YA MAHASIMU WAO SIMBA...!

Mashabiki wa Yanga walivyokuwa wakionekana kwenye mitaa ya jiji la Tanga kabla ya mechi yao dhidi ya Copastal Union ambayo Yanga walishionda 2-0. 

Biashara ya jezi za Yanga na vuivuzela za njano iliendelea katika mitaa mbaimbali jijini Tanga kabla ya mechi ya Yanga dhidi ya wenyeji Coastal Union kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini humo. Yanga ilishinda 2-0 kutokana na magoli ya Didier Kavumbagu na Hamis Kiiza.

Mashabiki wa Yanga wakiwa katika eneo la stendi kuu ya mabasi jijini Tanga

Mashabiki wengine jijini Tanga walitupia jezi za Yanga kumtania mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage kama huyu anayeonekana kushoto.

Hapa waligongana mashabiki wa Yanga na Coastal katika eneo la Stendi Kuu ya mabasi jijini Tanga.

Mashabiki Yanga wakitamba na ngoma zao.


Ilikuwa ni burudani ya aina yake jijini Tanga wakati mashabiki wakiendeleza vijembe kabla ya mechi kati ya Yanga na Coastal Union. Yanga ilishinda 2-0.


Ni ngoma na vuvuzela kwa kwenda mbele.





Mashabiki wengine walisafiri kwa mabasi kutoka jijini Dar es Salaam hadi jijini Tanga kuishangilia timu yao. Hawa ni Wazee wa Mipango kutoka Keko, Temeke.




Baadhi ya mashabikii wa Yaga wakipata msosi kabla ya kwenda uwanjani kuishangilia timu yao.

Mashabiki walikuwa wametapakaa katika mitaa mingi jijini Tanga kabla ya pambano la Yanga dhidi ya wenyeji Coasta.

Hapa kulikuwa na mchangayiko wa mashabiki wa Yanga na Coastala.


Hapa sasa nbi nje ya Uwanja wa Mkwakwani... mashabiki wakiwa mbioni kuingia uwanjani kushuhudia mechi ya Yanga dhidi ya wenyeji Coastal Union.

Yanga tutashinda 3-0...! Ndivyo shabiki huyu alivyokuwa akitabiri kabla ya kuanza kwa mechi yao dhidi ya Coastal kwenye Uwanja wa Mkwakwani. Hata hivyo, Yanga walishinda 2-0. 









Kama kawa jijini Tanga... mashabiki wengi walifika kwenye Uwanja wa Mkwakwani wakiwa na baiskeli.

Kama Yanga na Simba vile....! Yanayoonekana kwa mbali eneo la kupaki magari ndani ya Uwanja wa Mkwakwani ni basi la Yanga (kushoto) na la Coastal linaloonyesha nembo ya wadhamini wao kampuni ya Tanga Cement.

Mgambo JKT pia walikuwapo... hili ndilo basi lao lililowaleta uwanjani. 
 
Eneo hili walijaa mashabikji wa Yanga... ilikuwa ukionekana na jezi ya rangi nyekundu na nyeupe ya Coastal umeondolewa kwa kubebwa juujuu! 

Eneo hili walijaa mashabikji wa Coastal... ilikuwa ukionekana na jezi ya rangi ya njano na kijani ya Yanga; umeondolewa kwa kubebwa msobemsobe! 

Dah... nd'o basi tena! Mashabiki wa Coastal wakiwamo baadhi ya 'watasha' waliojichanganya nao wakionekana kukata tamaa baada ya kutanguliwa na Yanga kwa mabao 2-0 huku dakika zikiyoyoma ndani ya Uwanja wa Mkwakwani.

Baadhi ya vigogo wa Yanga waliwepo uwanjani kuipa sapoti timu yao wakati ikicheza dhidi ya Coastal na kushinda 2-0... kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrance Mwalusako, Makamu Mwenyekiti Clement Sanga na wajumbe wa kamati mojawapo ya Yanga, Davis Mosha (anayepiga makofi).







No comments:

Post a Comment