Wednesday, November 14, 2012

MTAZAME CRISTIANO RONALDO ANAVYOONEKANA BAADA YA KUPASULIWA JUU YA JICHO...MWENYEWE AONDOA HOFU MASHABIKI WAKE NA KUSEMA ATARUDI UWANJANI HARAKA HUKU AKIWA 'FITI' 100%...!

Sasa niko poa...! Ronaldo anavyoonekana katika picha yake aliyoiweka katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook.
STRAIKA wa kimataifa wa Ureno na klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo amewashukuru mashabiki kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Facebook na kuwaambia kuwa wasiwe na wasiwasi kuhusiana na jeraha alilopata Jumapili la juu ya jicho kwani sasa yuko 'fiti' na atakuwa tayari kuichezea klabu yake mwishoni mwa wiki. 

Cristiano ameandika: "Najihisi vizuri na natumai kuwa nitarejea uwanjani haraka."

Nyota huyo Mreno ameweka pia picha yake kwenye ukurasa wake wa Facebook, akimbatanisha na maelezo ya picha ambayo yanawashukuru mashabiki kwa kumuunga mkono wakati wote: "Ahsante kwa salamu za kunitakia kheri mlizonitumia tangu siku nilipoumia. Najihisi vizuri na, natumai kurudi uwanjani mara moja nikiwa fiti kwa 100%".

No comments:

Post a Comment