Saturday, October 6, 2012

MKENYA MARIGA AFUKUZIWA NA FULHAM, READING...!

MacDonald Mariga.

MacDonald Mariga wa Inter Milan akishangilia baada ya kufunga goli la tatu dhidi ya Genoa kuwania Kombe la Tim kwenye Uwanja wa Giuseppe Meazza mjini Milan,  Januari 12, 2011.
MILAN, Italia
Kiungo wa klabu ya Inter Milan inayoshiriki Serie A, Ligi Kuu ya Italia, Mkenya  McDonald Mariga anafukuziwa na klabu kadhaa za Ligi Kuu ya England zikiwamo za Fulham na Reading, imefahamika.

Gazeti la Tuttosport limesema leo kuwa Fulham na Reading zinajiandaa kumfukuzia kiungo huyo wa timu ya taifa ya Kenya 'Harambee Stars' wakati wa dirisha dogo la usajili wa Januari.

Inadaiwa kuwa Inter imepokea ofa kadhaa za kumsajili kiungo huyo mwenye miaka 25, zikiwamo za Fulham na Reading.

No comments:

Post a Comment