Tuesday, October 9, 2012

MISS MBULU AWA WA KWANZA KUINGIA 16-BORA REDDS MISS TANZANIA 2012

Lucy Stephano akifurahi baada ya kutangazwa mshindi wa taji dogo la Redd's Miss Photogenic 2012 wakati wa shindano hilo lililofanyika jana usiku kwenye ukumbi wa hoteli ya E'Manyata Lodge, Monduli jijini Arusha. Picha: Intellectuals Communications Limited
Lucy Stephano akifurahi baada ya kutangazwa mshindi wa taji dogo la Redd's Miss Photogenic 2012 wakati wa shindano hilo lililofanyika jana usiku kwenye ukumbi wa hoteli ya E'Manyata Lodge, Monduli jijini Arusha. Picha: Intellectuals Communications Limited

Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino Agency na muandaaji mkuu wa Mashindano ya Miss Tanzania, Hashim Lundega (kulia) akitangaza mshindi wa Redd's Miss Photogenic ambaye ni mshiriki kutoka Manyara - Kanda ya Kaskazini, Lucy Stephano (katikati) wakati wa shindano hilo dogo lililofanyika jana usiku kwenye ukumbi wa hoteli ya E'Manyata Lodge, Monduli jijini Arusha.

Lucy Stephano (wa tatu kulia) akishangilia baada ya Lundenga (kulia) kutangazwa mshindi wa taji dogo la Redd's Miss Photogenic 2012 wakati wa shindano hilo lililofanyika jana usiku kwenye ukumbi wa hoteli ya E'Manyata Lodge, Monduli jijini Arusha. Picha: Intellectuals Communications Limited

Lucy Stephano akipongezwa wenzake baada ya kutangazwa mshindi wa taji dogo la Redd's Miss Photogenic 2012 wakati wa shindano hilo lililofanyika jana usiku kwenye ukumbi wa hoteli ya E'Manyata Lodge, Monduli jijini Arusha. Picha: Intellectuals Communications Limited

Warembo walioingia kwenye hatua ya Tano Bora ya Redd's Miss Photogenic kutoka kulia ni Magdalena Roy (Dar City Center - Kanda ya Ilala), Babylove Kalala (Kagera - Kanda ya Ziwa), Lightness Michael (Dodoma - Kanda ya Kati), Lucy Stephano (Manyara - Kanda ya Kaskazini) na Diana Hussein (Dar Indian Ocean - Kanda ya Kinondoni) wakipozi wakati wa shindano hilo

Na Mwandishi Wetu, Monduli
LUCY Stephano ambaye ni Redds Miss Mbulu jana usiku alikuwa mshiriki wa kwanza kuingia katika hatua ya 16-Bora ya Redd’s Miss Tanzania 2012 baada ya kutwaa taji la Redds Miss Photogenic katika shindano lililofanyika kwenye Ukumbi wa Emanyata Lodge, uliopo mjini hapa.

Lucy aliwashinda warembo wengine 30 wanaoshiriki Redds Miss Tanzania na kufanikiwa kutwaa taji hilo.

Mrembo huyo alitwaa taji hilo baada ya ushindani mkali uliokuwepo kati yake na Redds Miss Dar Indian Ocean, Diana Hussein na Redds Miss Ilala namba mbili, Magdalena Roy.

Kutokana na kutwaa taji hilo, Lucy amepiga hatua moja kubwa zaidi kuelekea taji la Redds Miss Tanzania 2012 linalotarajiwa kufanyika Novemba 3, mwaka huu.

Mrembo mwingine anayetarajiwa kuingia hatua hiyo atapatikana Jumamosi katika ‘Usiku wa Redd’s Miss Tanzania’ mjini Arusha pale vimwana watakapochuana katika kinyang’ayiro cha Miss Top Model.

Shindano la Redd’s Miss Tanzania kwa sasa linadhaminiwa na kinywaji cha Redd’s Original kinachozalishwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).

No comments:

Post a Comment