Saturday, October 27, 2012

MIKEL ARTETA AFUNGA BAO PEKEE LEO KUIPA ARSENAL USHINDI WA 1-0 DHIDI YA QPR... KIUNGO JACK WILSHERE WA ARSENAL ACHEZA KWA DAKIKA 67 BAADA YA KUWA NJE YA UWANJA KWA MIEZI 17...WIGAN YAIUA WEST HAM UNITED 2-1

Weweeeeeeeee....! Mikel Arteta akishangilia baada ya kufunga goli la pekee dhidi ya QPR wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya England kwenye Uwanja wa Emirates leo, Oktoba 27, 2012.
Mikel Arteta wa Arsenal akipiga mpira unaompita kipa Ryan Nelsen wa QPR na kufunga wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya England kwenye Uwanja wa Emirates mjini London leo, Oktoba 27, 2012.
Goooooohh...! Aaron Ramsey (Na.16) wa Arsenal akishangilia goli lililofungwa na mchezaji mwenzake wa Arsenal, Mikel Arteta (Na. 8) wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya England kwenye Uwanja wa Emirates mjini London leo, Oktoba 27, 2012.
Sasa hivi natisha kinoma...! Jack Wilshere wa Arsenal akiwatoka Shaun Wrights Phillip na Esteban Granero wa QPR wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya England kwenye Uwanja wa Emirates leo, Oktoba 27, 2012.

Wilsherer wa Arsenal (kulia) akifanya vitu vyake leo, Oktoba 27, 2012
Kashakash langoni mwa Wigan wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya England dhidi ya West Ham United leo, Oktoba 27, 2012.

Niache huko...! Hapa ni mshikemshike katika mechi ya Ligi Kuu ya England kati ya Stoke na Sunderland leo, Oktoba 27, 2012.



LONDON, England
Goli la 'usiku' lililofungwa na Mikel Arteta mwishowe lilihitimisha ugumu wa klabu ya mkiani mwa msimamo wa ligi ya QPR wakati Arsenal ilipojipoza kutokana na matokeo mabaya waliyopata katikati ya wiki kwa ushindi muhimu wa 1-0 katika Ligi Kuu ya England leo.

Arteta alifunga kwa shuti la karibu kabisa na lango, baada ya mpira wake wa kwanza aliopiga kichwa kugonga 'besela' langoni mwa QPR, wakati Arsenal ikirejea kwenye mstari baada ya vipigo viwili mfululizo walivyopata kutoka kwa Norwich na Schalke.

Ushindi huo wa Arsenal iliyomiliki mpira kwa asilimia 70 ulipatikana baada ya Stephane M'Bia wa QPR kutolewa nje kwa kadi nyekundu kufuatia kosa lake la kumpiga teke Thomas Vermaelen wa Arsenal.

Esteban Granero wa QPR na mwenzake Jamie Mackie walipoteza nafasi za wazi kuisawazishia timu yao.

Kiungo wa timu ya taifa ya England, Jack Wilshere alicheza kwa dakika 67 wakati alipoichezea timu ya wakubwa ya Arsenal kwa mara ya kwanza baada ya kuwa nje kwa miezi 17 kutokana na majeraha.

Hata hivyo, ushindi huo haukuisadia Arsenal kupanda zaidi bali imebaki katika nafasi yake ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England baada ya kufikisha pointi 15; huku Chelsea (pointi 22), Man U (pointi 19) na Man City (pointi 18) zikiendelea kushika nafasi tatu za juu.

Matokeo mengine ya mechi za leo za Ligi Kuu ya England:
•    Aston Villa 1 - 1 Norwich
•    Reading     3 - 3 Fulham
•    Stoke         0 - 0 Sunderland 
•    Wigan        2 - 1 West Ham 

MSIMAMO WA LIGI KUU ENGLAND BAADA YA MECHI ZA LEO JIONI:



P
   GD   
Pts
Iko palepale  1
8
   13
22
Imepanda       2
9
   8
19
Imeshuka       3
8
  10
18
Iko palepale   4
9
  8
15
Iko palepale  5
8
  6
15
Iko palepale  6
9
  5
14
Iko palepale  7
8
  3
14
Iko palepale  8
8
  3
14
Iko palepale  9
9
  2
14
Iko palepale  10
9
  2
12
Iko palepale  11
8
 -3
10
Iko palepale  12
9
 -1
9
Iko palepale  13
8
 -2
9
Iko palepale  14
8
 -2
9
Iko palepale  15
9
 -6
8
Iko palepale  16
9
 -11
7
Iko palepale  17
9
 -7
6
Iko palepale  18
8
 -6
4
Iko palepale  19
8
 -11
4
Iko palepale  20
QPR
9
-11
3


No comments:

Post a Comment