Tuesday, October 16, 2012

BRAZIL YAWAUA JAPAN 4-0 LEO.... KAKA ANG'ARA NA KUFUNGA MOJA, NEYMAR AFUNIKA PIA NA KUTUPIA 2

Neymar (kushoto) akichuana na mchezaji wa Japan leo.
Huniwezi dogo...! Hulk akimtoka beki wa Japan wakati wa mechi yao ya kimataifa ya kirafiki waliyocheza nchini Poland, leo Oktoba 16, 2012. 
Sylva na Luiz wa Brazil wakipongezana wakati wa mechi yao ya kimataifa ya kirafiki waliyocheza dhidi ya Japan nchini Poland, leo Oktoba 16, 2012. 

Beki Yasuyuki Konno wa Japan akichuana na Neymar wa Brazil  wakati wa mechi yao ya kimataifa ya kirafiki waliyocheza nchini Poland, leo Oktoba 16, 2012. 
Yalaaa...!

Tunatishaaaaaa....! Wachezaji wa timu ya taifa ya Brazil wakipongezana baada ya kumalizika kwa mechi yao ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya Japan iliyochezwa nchini Poland leo na kuibuka na ushindi wa 4-0.
 POZNAN, Poland
Brazil walitawala mechi nzima waliyocheza ugenini kuanzia saa 9:10 alasiri leo na kushinda 4-0 katika mechi yao ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya Japan mjini  Poznan, Poland leo Jumanne.

Paulinho alifunga goli la utangulizi katika dakika ya 12 kutokana na shuti kali alilopiga kutoka umbali wa yadi 20, kabla Neymar hajaongeza la pili kwa njia ya penati katika dakika ya 29.

Katika kipindi cha pili, Brazil waliongeza mashambulizi na straika wa Santos, Neymar akafanya ubao wa magoli usomeke 3-0, kabla Kaka aliyeonyesha kiwango cha juu hajafunga bao la nne kuelekea mwisho wa mechi hiyo.

Kaka alianza tena kikosini katika kikosi kilichoonekana kuwa ni kile kile cha kocha Mano Menezes, ambaye alibadili mchezaji mmoja tu kutoka katika timu iliyoanza dhidi ya Iraq na kushinda 6-0, akianza Leandro Castan badala ya majeruhi Marcelo.

No comments:

Post a Comment