BARCELONA, Hispania
Kocha wa Barcelona,
Tito Vilanova amekanusha taarifa kwamba kuna bifu kali kati ya David Villa na
Lionel Messi.
Wawili hao
walionekana wakibwatukiana wakati wa mechi yao ya La Liga, Ligi Kuu ya Hispania
waliyoshinda 2-0 dhidi ya Granada jana.
"Hakuna kitu
chochote (kilichotokana na kubwatukiana kati ya Villa na Messi)," Vilanova
amesema wakati wa mkutano na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa mechi.
"Yeyote
aliyewahi kucheza soka anajua kwamba kujibishana ni kitu cha kawaida, na pia ni
sehemu ya mchezo.
"Matukio kama
yale ni dalili kwamba timu iko hai. Kutoambiana kitu kwa manufaa ya timu
kunamaanisha kwamba kuna tatizo kubwa".
No comments:
Post a Comment