Monday, September 24, 2012

MECHI YA REA MADRID, RAYO VALLECANO KUCHEZWA LEO SAA 2:45 USIKU KWA SAA ZA KIBONGO... NI BAADA YA KUAHIRISHWA KUFUATIA HUNI MOJA KUKATA NYAYA ZA TAA UWANJANI JANA USIKU NA KUSABABISHA BONGE LA GIZA!

Cristiano Ronaldo wa Real Madrid akishangilia baada ya kufunga goli lililowapa ushindi wa 1-0 dhidi ya Rayo Vallecano wakati wa mechi yao ya La Liga kwenye Uwanja wa Teresa Rivero,  Februari 26, 2012.
Alvaro Arbeloa wa Real Madrid (kushoto) na kocha msaidizi wa klabu hiyo, Aitor Karanka wakisubiri refa kuahirisha mechi yao iliyokuwa ichezwe jana usiku dhidi ya Rayo Vallecano baada ya nusu ya uwanja kukabiliwa na giza kufuatia hujuma iliyofanywa na mtu asiyefahamika kwenye Uwanja wa Teresa Rivero jana. Mechi hiyo sasa itachezwa leo saa 2:45 usiku. Picha: REUTERS
MADRID, Hispania
Real Madrid wamekubali kwa mbinde kucheza mechi yao ya ugenini ya La Liga, Ligi Kuu ya Hispania dhidi ya Rayo Vallecano leo kuanzia saa 2:45 usiku, ikiwa ni siku moja tu baada ya mechi yao kuahirishwa kwa sababu ya mtu asiyefahamika kukata nyaya za umeme za taa za Uwanja wa Rayo wa Vallecas na kusababisha giza.

Mechi hiyo ilikuwa ichezwe jana kuanzia saa 4:30 usiku lakini uwanja ulikuwa nusu-giza na mashabiki walikuwa bado wakisubiri nje ya milango iliyokuwa imefungwa kuwapiosha mafundi waliokuwa wakiendelea na matengenezo.

Rais wa Rayo, Raul Martin Presa amesema kuwa mtu huyo asiyefahamika amekata nyaya za baadhi ya taa na wakati tatuzo hilo lilipogundulika, hawakuweza kufanya lolote kwani tayari mechi hiyo ilishaahirishwa.

Awali, Real walisema kwamba hawataki tena kukumbana na tatizo hilo la taa za uwanjani na kupendekeza kuwa mechi hiyo ichezwe leo kuanzia saa 12:00 jioni (kwa saa za Kibongo), wakati Rayo wakisisitiza kwamba ichezwe kuanzia saa 3:00 usiku (kwa saa za Kibongo) ili kutoa nafasi kwa mashabiki wengi zaidi wa Rayo kuhudhuria.

Hata hivyo, mwishowe waendeshaji wa La Liga walikubaliana na pande zote mbili -- Real Madrid na Rayo Vallecano -- kuwa mechi hiyo ichezwe leo kuanzia saa 2:45 usiku (kwa saa za Kibongo).   

Rayo wakasema kuwa tiketi zilizokatwa kwa ajili ya mechi ya jana ndizo zitakazotumika leo na kwamba, mashabiki wasioweza kuhudhuria wanaweza kuzirejesha.

No comments:

Post a Comment