Saturday, August 4, 2012

YANGA YAMTAMBULISHA DIDIER KAVUMBAGU

Afisa Habari wa Yanga, Loius Sendeu (katikati) akishika jezi Na.21 itakayovaliwa na mshambuliaji mpya wa klabu hiyo, Didier Kavumbagu (kulia). Kushoto ni mshambuliaji wa Yanga, Said Bahanunzi. 

MSHAMBULIAJI wa kimataifa kutoka timu ya Olympic Atletico ya Burundi, Didier Kavumbagu amewasili jana usiku na kujiunga na kikosi cha mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati Young Africans Sports Club tayari kwa kuanza kuitumikia timu yake mpya.

Didier Kavumbagu aliichezea timu ya Olympic Atletico katika mashindano ya Kagame ya mwaka huu na kuifikisha timu yake hatua ya Robo Fainali, kabla ya kutolewa na timu ya URA ya Uganda.

Pamoja na timu yake kutolewa katika hatua ya robo fainali, Didier alionyesha kiwango cha hali ya juu ikiwa ni pamoja kufunga mabao yote mawili katika mchezo wa kwanza wa ufunguzi wa mashindano ya Kagame dhidi ya Young Africans.

Mchezaji huyo wa timu ya Taifa ya Burundi amesajliwa kuichezea timu ya Young Africans kwa mkataba wa miaka miwili ambapo atakua mitaa ya Twiga na Jangwani hadi mwishoni mwa msimu wa 2013-2014.

Kavambagu alizaliwa tarehe 02/05/1988 mjini Bujumbura na kuanza kucheza soka katika timu za mitaani kabla ya kuchaguliwa timu ya taifa ya vijana U-17 mwaka 2006 na kushiriki mashindano ya kombe la vijana CECAFA U-17 visiwani Zanzibar.

Alionyesha kiwango cha hali ya juu katika mashindano hayo na kupelekea kusajiliwa na timu ya Olympic Atletico ambapo ameitumikia mpaka mwaka huu alipoamua kuachana na yo na kujiunga na mabingwa wapya wa kombe la Kagame Young Africans Sports Club.

Young Africans imeanza jana mazoezi yake kwa ajiliya kujiandaa na msimu mpya wa ligi kuu Tanzania bara unaotazamiwa kuanza Septemba mosi, na wachezaji wote wamehudhuria mazoezi jana na leo Didier amejumuika na wachezaji wenzake kufanya mazoezi chini ya kocha Mbelgiji Tom Saintfiet katika uwanja wa shule ya sekondari Loyola.

CHANZO: http://youngafricans.co.tz

No comments:

Post a Comment