Monday, August 13, 2012

USAIN BOLT: CRISTIANO RONALDO NI MKALI KULIKO LIONEL MESSI

Ronaldo (kushoto) na Messi wakiwa hoi baada ya mechi mojawapo ya el clasicco kati ya timu zao za Real Madrdi na Barcelona.

Ronaldo akifurahia baada ya kuifungia bao Real Madrid

Messi akishangilia baada ya kuifungia Barca bao.
Usain Bolt
LONDON, England
MWANARIADHA nyota wa Jamaica, Usain Bolt amesema leo kuwa straika wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo ana kiwango cha juu zaidi cha soka na kwamba amemuacha mbali sana straika wa Barcelona, Lionel Messi.

Bolt na Ronaldo wana urafiki binafsi, ambao ulianza wakati Bolt alipokuwa akimpa Ronaldo mafunzo ya kukimbia wakati alipokuwa akiichezea Manchester United.

"Hakuna swali, Cristiano ni mkali kuliko Messi. Yeye ni mchezaji aliyekamilika zaidi," anasema Bolt. 


"Cristiano ni mcheshi na pia ni mtu safi sana," anaongeza Bolt.

No comments:

Post a Comment