Monday, August 13, 2012

JOE HART, STURRIDGE WATEMWA TAIFA ENGLAND


Daniel Sturridge

Joe Hart
LONDON, England
KIPA Joe Hart na straika Daniel Sturridge hawatakuwamo katika kikosi cha timu ya taifa ya England kitakachocheza mechi ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya Italia keshokutwa kutokana na majeraha.

Hart, kipa wa Manchester City ambaye ni chaguo la kwanza katika timu ya taifa, hakuwamo pia katika kikosi cha klabu yake kilichoshinda 3-2 dhidi ya Chelsea jana na kutwaa Ngao ya Jamii kutokana na maumivu ya mgongo.

Hata hivyo, kocha wake Roberto Mancini alisema kuwa tatizo alilo nalo "sio kubwa sana."

Straika wa Chelsea, Sturridge aliumia kidole gumba cha mguu wakati alipoingia akitokea benchi kwenye uwanja wa Villa Park.

Kocha wa timu ya taifa ya England, Roy Hodgson hajaita mchezaji mwingine yeyote kuziba nafasi za wawili hao, na hivyo John Ruddy wa Norwich City atakuwa akipigania nafasi ya kuitwa kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa mjini Berne, pamoja na kipa Na.1 wa timu ya England iliyoshiriki michezo ya Olimpiki, Jack Butland.

Andy Carroll, Jermain Defoe na Theo Walcott ndio washambuliaji waliobaki kikosini. Mechi hiyo itakayochezwa kwenye uwanja huru ni marudio ya robo fainali ya michuano ya Euro 2012 iliyoandaliwa na nchi za Poland na Ukraine, ambapo kikosi cha kocha Cesare Prandelli kiliifunga England kwa penati kabla na kutinga fainali.

No comments:

Post a Comment