Monday, August 13, 2012

TUMEKOSA MEDALI OLIMPIKI LAKINI KWA SARAKASI TUMETESA

Watanzania wa kikundi cha sarakasi cha Black Eagles wakibeba mwenge wa Olimpiki wakati wa shamrashamra za Michezo ya Olimpiki ya London 2012.
Wacheza sarakasi wa kikundi cha Black Eagles wakifanya mambo nchini Uingereza

Wacheza sarakasi wa kikundi cha Black Eagles wakifanya mambo nchini Uingereza

Wacheza sarakasi wa kikundi cha Black Eagles wakipozi kwa picha
WAKATI timu ya Olimpiki ya Tanzania imeshindwa vibaya katika Michezo ya London 2012, faraja pekee inaweza kuwa ni kundi la sanaa Black Eagles Acrobatics linaloundwa na Watanzania waishio Chatham Kent, Uingereza, ambalo liliakwa kutumbuiza kwenye shamrashamra za michezo hiyo ya London.

Mkurugenzi wa kundi hilo Ally Kasele alisema kuwa ni fahari Black Eagles kualikwa na kufanya sarakasi mbele ya maelfu ya watu waliomiminika nchini Uingereza kuhudhuria Michezo ya Olimpiki.


"Walialikwa wasanii zaidi ya 200 kutoka nchi mbalimbali na sisi kutoka Tanzania tulikuwa miongoni mwao… hii ilikuwa ni fahari kwetu kuitangaza nchi yetu," alisema Kasele.


Alisema kuwa walipangiwa kufanya vitu vyao kila kona ya eneo la Olimpiki Park na kushangiliwa sana na maelfu ya watu kwa maajabu waliyokuwa wakiyafanya huku waandaji nao wakibaki wameduwaa kwa vitu vyao.
"Waandaji hao walisikika wakisema kuwa Black Eagles tumekuwa wa kwanza kwa kuwapagawisha mashabiki hadi wakaturuhusu kwenda kushika Mwenge wa Olimpiki," alisema.


Aidha, alisema mwaka huu kundi hilo limefanya maonyesho mbalimbali yakiwamo ya kukimbiza Mwenge wa Olimpiki kwenye maeneo ya Kennington, London, Derby, Newbur Berkshire, City Centre Cardiff, Dulston London na Hackney na kujizolea umaarufu.


"Mbali na maonyesho hayo, tulishashiriki pia Jubilee ya Malkia ya Uingereza ambayo inajulikana kama Queen's Jubilee hali ambayo ilichangia kutuongezea umaarufu na kutufanya tujulikane zaidi hapa Uingereza," alisema.
Kasele alisema kuwa kundi hilo lina wasanii 16 na kuwataja baadhi yao kuwa ni yeye (Kasele) mkurugenzi, Simon Thobias, Mohamed Idd, Hilary Majaliwa na Shaban.


Alifafanua kuwa The Black Eagles Acrobatics lilianzishwa mwaka 1996 na limekuwa pia likipokea wasanii mbalimbali kutoka Tanzania ambao hufika Uingereza kushiriki maonyesho mbalimbali yakiwemo ya Sikukuu ya Krismasi.

No comments:

Post a Comment