Saturday, August 18, 2012

KIJANA 'ALIYEOKOTWA' NA KULELEWA NA WHITNEY, AMBAYE SASA ANATOKA NA BINTI WA BOBBY BROWN, BOBBI KRISTINA

Bobbi Kristina Brown, binti wa muimbaji marehemu Whitney Houston, akionyesha tattoo yake yenye herufi za kwanza "W H" wakati akipungia alipokuwa akiwasili na boifrendi wake Nick Gordon kwenye uzinduzi wa filamu ya "Sparkle" iliyomshirikisha Jordin Sparks na Whitney Houston (filamu yake ya mwisho kabla hajafariki) mjini Hollywood juzi Agosti 16, 2012. Gordon alichukuliwa na Whitney kwa ajili ya kulelewa nyumbani kwa nyota huyo kutokana na matatizo katika familia yao lakini sasa amekuwa boifrendi wa Bobbi Kristina. Picha: REUTERS
Bobbi Kristina Brown, binti wa muimbaji marehemu Whitney Houston, akipungia wakati alipowasili na boifrendi wake Nick Gordon kwenye uzinduzi wa filamu ya "Sparkle" iliyomshirikisha Jordin Sparks na Whitney Houston (filamu yake ya mwisho kabla hajafariki) mjini Hollywood juzi Agosti 16, 2012. Gordon alichukuliwa na Whitney kwa ajili ya kulelewa nyumbani kwa nyota huyo kutokana na matatizo katika familia yao lakini sasa amekuwa boifrendi wa Bobbi Kristina. Picha: REUTERS

NICK Gordon (22) na Bobbi Kristina (19) wameishi pamoja kwa zaidi ya miaka 10 kama kaka na dada kabla ya kifo cha Whitney Houston.

Kwa mujibu wa TMZ, Bobbi na Nick walilelewa pamoja baada ya Whitney kumchukua akiwa na umri wa miaka 12 wakati baba wa Kick alipohukumiwa kwenda gerezani na mama yake kushindwa kumlea.

Nick alikuwa ni mtoto wa kuasili wa Whitney japo hakumuasili rasmi kisheria, na alikuwa akimchukulia kama mwanae mpaka muimbaji huyo alipofariki akiwa na umri wa miaka 48 kutokana na kuzama kwa bahati mbaya bafuni kulikotokana na matatizo ya moyo yaliyosababishwa na utumiaji wa dawa za kulevya.

Lakini Bobbi Kristina Brown sio tu kwamba alionekana akimbusu kimahaba kaka yake huyo aliyegeuka kuwa mpenziwe, bali pia alituma ujumbe kwenye ukurasa wake wa Twitter akielezea namna anavyompenda mwanaume huyo, huku kidoleni akuonekana na pete ya uchumba.

'Sababu 1 ya mimi kuwa na tabasamu leo.:) nakupendaa booboo, milele & daima. Ni SISI tu sasa"...@Nickdgordon', Bobbi Kristina aliandika katika ukurasa wake wa Twitter huku aki-post na picha inayomuonyesha akimbusu Nick.

Picha iliyotumwa kwenye Twitter na Bobbi Kristina inayomuonyesha akimbusu kaka yake aliyegeuka mchumba wake

Mvulana huyo alichochea uvumi kuhusu mahusiano yao kwa kutuma ujumbe katika Twitter mwezi Machi mwaka huu, akisema: 'Yea tumezidi kuwa karibu sasa nini kinafuata!!!'

Bobbi Kristina akiwa na kaka yake aliyegeuka mpenzi wake Nick Gordon wakati wa kumbukumbu ya kutimiza miaka 49 ya Whitney Houston

Wapenzi hao wameripotiwa kuendelea kuishi pamoja katika jumba la Whitney tangu alipofariki muimbaji huyo lenye thamani ya dola milioni 1.2 lililopo mjini Atlanta.

Bibi wa Bobbi Kristina, Cissy Houston, amepinga mahusiano hayo.


No comments:

Post a Comment