Saturday, August 18, 2012

ONA JINSI VAN PERSIE ALIVYOKUWA AKILA BATA NA FAMILIA YAKE KATIKA VISIWA VYA PITIUSIC KABLA YA KUITOSA ARSENAL NA KUTUA MANCHESTER UNITED

Hee...! Nini tena? Van Persie na mkewe Bouchra wakicheza ndani ya maji
Kama dolphin... mke wa Van Persie akionyesha umahiri wa kupiga mbizi huku mumewe akicheza binti yao, Dina. Bikini hii aliyotupia Bouchra ni aina ya Gucci na bei yake dukani ni paundi  za England 280 (Sh. 700,000). Hapa ilikuwa mwaka juzi.

Chu-chu-chuuu...! Van Persie akicheza majini na binti yake, Dina kwenye visiwa vya Pitiusic, mwaka juzi.

Angalia kuleee....! Van Persie akipata maelekezo kutoka kwa mkewe Bouchra kwenye visiwa vya Pitiusic, mwaka juzi.  

Fumba macho...! Van Persie akimsikiliza mkewe Bouchra huku pembeni wakiwa na mpambe aliyembeba mtoto wao wa kiume, Shaquille.  Hii ilikuwa mwaka juzi

Daddy na mie taka piga mbizi...! Van Persie akicheza majini na mkewe Bouchra na watoto zao Dina na Shaquille, kwenye visiwa vya Pitiusic mwaka juzi. Miwani ya jua aliyovaa Bouchra ni aina ya Tom Ford.



Bouchra... mke wa Van Persie
Mmmmwaaaa... ndio kuna mtoto lakini hayakuhusu!!

Van Persie akiwa na binti yake, Dina katika fukwe za visiwa vya Pitiusic 

Daddy nishushe... Van Persie na binti yake Dina wakiwa kwenye fukwe za visiwa vya Pitiusic, Julai 14, 2012

Taratibu...!

Safari imeanza... Van Persie, mkewe Bouchra na watoto wao Shaquille na Dina wakiwa ndani ya boti ndogo kwenye fukwe za visiwa vya Pitiusic, Julai 14, 2012

Sweetie wakubalie Man U tupate mijihela kuliko ya Arsenal...Van Persie, mkewe Bouchra na watoto zao Dina na Shaquille wakiwa ndani ya boti ndogo wakati wakila bata kwenye visiwa vya Pitiusic, Julai 14, 2012

Lazima niondoke Arsenal...Van Persie akionekana mtulivu wakati yeye na familia yake wakiponda maraha kwenye visiwa vya Pitiusic, Julai 14, 2012

Hapa ni Van Persie, familia yake na wapambe.... ndani ya boti kwenye visiwa vya Pitiusic, Julai 14, 2012

Van Persie na mkewe Bouchra

Twenzetu...! Van Persie na mkewe Bouchra wakiwa tayari kwa mtoko
MANCHESTER, England
 Wakati akiwa akiichezea klabu ya Arsenal, Robin van Persie alikuwa amejenga mazoea ya kuambatana na familia yake kwenda kuponda maraha katika visiwa vya Pitiusic vilivyopo nchini Hispania.

Kila alipokuwa katika mapumziko marefu ya msimu, Van Persie na familia yake hawakuwa wakijiweka nyuma. Walikwenda sehemu mbalimbali zenye utulivu na kujiachia kiasi cha kutosha.

Karibu nusu ya mwezi ulipita, straika huyo aliyekamilisha uhamisho wa kwenda Manchester United akitokea Arsenal kwa ada ya paundi za England milioni 24 (Sh. bilioni 60), aliongozana na mkewe Bouchra na watoto wao Shaquille na Dina kwenda kufaidi maisha katika fukwe za visiwa hivyo vya Pitiusic, wakiambatana pia na swahiba zao kadhaa.

Van Persie na familia yake walionekana ufukweni wakitabasamu muda wote; wakila, kunywa, kuchezea maji na kujianika juani kadri walivyotaka.

Uhamisho wa kwenda Man U mwishoni mwa wiki umemhakikishia 'mafweza' zaidi mifukoni mwake na pengine kuwafanya mkewe na wanawe wafaidi zaidi maisha; kwani imeelezwa kuwa katika mkataba wake wa miaka minne, sasa straika huyo wa kimataifa wa Uholanzi atakuwa akilipwa mshahara mnono wa paundi za England 250,000 kwa wiki, sawa na Sh. milioni 615!

Je, kwanini Van Persie na familia yake wasiendelee kufaidi maisha katika maeneo ghali kama ya visiwa vya Pitiusic?

No comments:

Post a Comment