Monday, August 13, 2012

ARSENAL WATAKA BILIONI 50/- WAMUACHIE WALCOTT KWA MAN CITY, CHELSEA, LIVERPOOL AU INTER MILAN

Theo Walcott ... akichomoka na mpira kwa kasi kama ya Usain Bolt kuelekea lango la wapinzani. Pamoja na makali yake yote, bado Arsenal ya kocha Arsene Wenger iko tayari kumuuza kwa timu yoyote itakayokuwa tayari kuweka mezani 'bulungutu' la Sh. bilioni 50!
Hapa Theo Walcott akimlamba chenga beki wa timu ya Kitchee FC ya Hong Kong kabla ya kufyatuka kwa mibio yake ya kasi ya umeme wakati wa mechi yao ya kirafiki kujiandaa na msimu mpya iliyochezwa jijini Hong Kong Julai 29, 2012 .  

LONDON, England
Arsenal wanataka walipwe mabilioni ya pesa ili kumuachia straika wao Theo Walcott aende kuichezea klabu yoyote kati ya zile zilizoonyesha dhamira ya kumuhitaji.

Taarifa kutoka ndani ya Arsenal zimefichua jioni hii kwamba Arsenal wako tayari kumuachia winga huyo mwenye kasi anayeichezea pia timu ya taifa ya England kwa dau lisilopungua paundi za England milioni 20, ambazo ni sawa na takriban Sh. bilioni 50.

Walcott yuko katika mwaka wa mwisho wa kumalizia mkataba wake wa sasa na tayari klabu kadhaa kubwa za Ulaya zimekuwa zikimfukuzia kwa udi na uvumbi ili kumng'oa kutoka mikononi mwa kocha Arsene Wenger, baadhi ya klabu hizo zikiwa ni za Chelsea, Liverpool, Manchester City na Inter Milan ya Italia.

Vyanzo vimedai kuwa tayari Inter wameshaiendea Arsenal na kuuliza bei ya nyota huyo ambapo jibu walilopewa ni hilo la kutakiwa 'kukata mkwanja' wa Sh. bilioni 50.

No comments:

Post a Comment