Monday, August 13, 2012

XABI ALONSO AGOMEA MAZUNGUMZO MKATABA MPYA REAL MADRID



Xabi Alonso
MADRID, Hispania
KUNA taarifa zilizopatikana leo zinazodai kuwa kiungo Xabi Alonso ametishia kutofanya mazungumzo ya kusaini mkataba mpya wa kuendelea kuichezea klabu yake ya Real Madrid.

Gazeti la Sport limesema kwamba  sasa Xabi anafikiria kuhitimisha kipindi chake cha kuichezea Real baada ya kumalizika kwa msimu ujao.

Mkataba wa sasa wa kiungo huyo mchezeshaji aliyewahi kuichezea pia Liverpool unamfunga Real  hadi mwaka 2014 na licha ya kufurahia maisha kwa vigogo hao wa Hispania, lakini anaamini kwamba sasa kipindi chake cha kung'ara kwenye klabu hiyo kinaelekea ukingoni.

Juventus na Inter Milan zimedaiwa kuanza kufuatilia kwa karibu maendeleo ya mazungumzo ya nyota huyo wa timu ya taifa ya Hispania na klabu yake ili ikibidi zianze harakati za kumtwaa.

No comments:

Post a Comment