Tuesday, July 31, 2012

WENGER: BENDTNER, PARK YOUNG RUKSA KUONDOKA ARSENAL

Niklas Bendtner

Park Young

Sebastien Squillaci
 LONDON, England
KOCHA Arsene Wenger wa Arsenal amesema kuwa wachezaji Niklas Bendtner, Park Young na Sebastien Squillaci wako mbioni kuondoka na kwamba pia atazungumza na winga Andrey Arshavin ili kuamua hatma yake klabuni hapo.

Arshavin ambaye ni straika mwenye miaka 31 alimalizia nusu ya pili ya msimu uliopita akiwa kwa mkopo katika klabu yake ya zamani ya Zenit St Petersburg ya Urusi, ikiwa ni baada ya kiwango chake kupondwa na mashabiki wengi wa Arsenal.

Zaidi ya hayo, nahodha huyo wa Urusi amekuwa akitarajiwa kuondoka kwenye klabu hiyo katika kipindi hiki cha majira ya kiangazi ili zipatikane fedha za kusajili nyota wengine zaidi baada ya kuwasili kwa wachezaji wapya Lukas Podolski na Olivier Giroud.

Hata hivyo, Wenger ahajafuta uwezekano wa kuendelea kumbakiza Arshavin, mchezaji aliyemnunua kwa paundi za England milioni 15 (Sh. bilioni 37) wakati wa usajili wa dirisha dogo la Januari, 2009, licha ya kwamba hakujumuishwa katika kikosi cha klabu hiyo kilichokwenda katika ziara yao ya Mashariki ya Mbali.

"Arshavin, inategemea. Tunapaaswa kukaa wote chini na kufanya mazungumzo. Anaweza kuendelea kuwa nasi klabuni," alisema Wenger kuiambia Daily Mail.

Wachezaji ambao hadi sasa wanaonekana kuwa ni mzigo katika kikosi cha Wenger ni pamoja na beki wa timu ya taifa ya Ufaransa, Sebastien Squillaci na mshambuliaji wa Korea Kusini Chu-Young Park, wote wakishindwa kuonyesha makali yao tangu walipotua wakitokea katika klabu za Sevilla na Monaco, wakati mshambuliaji wa kimataifa wa Denmark, Nicklas Bendtner, ambaye msimu uliopita aliichezea Sunderland kwa mkopo, pia yuko mbioni kuhama.

"Bendtner, Squillaci na Park wako njiani kuondoka na kwenda kucheza kwingine," aliongeza Wenger.

No comments:

Post a Comment