WACHEZAJI
11 wamemaliza mikataba yao ya kuichezea timu ya Coastal Union ya Tanga
inayoshiriki Ligi Kuu ya Tanzania Bara, na sasa wako huru kujiunga na
klabu yoyote.
Kwa
mujibu wa Coastal Union, wachezaji hao ni Ben Mwalala, Samwel Temu,
Francis Busungu, Ahmed Shiboli, Lawrence Mugia, Daudi Chengula, Godfrey
Mmasa, Mwinyi Abdulrahman, Sabri Ramadhan China, Soud Abdallah na
Ramadhan Wasso.
Uhamisho
wa wachezaji kwa msimu huu ulianza Juni 15 mwaka huu na utamalizika
Julai 30 mwaka huu wakati kipindi cha kuanza wachezaji (kwa wasio wa
Ligi Kuu) ni kati ya Juni 15 na 30 mwaka huu.
Kwa
klabu za Ligi Kuu kutangaza wachezaji watakaositishiwa mikataba yao ni
kuanzia Juni 15-30 mwaka huu na usajili wa wachezaji unafanyika kuanzia
Juni 15 hadi Agosti 10 mwaka huu.
No comments:
Post a Comment