Wednesday, July 4, 2012

KIMANJARO PREMIUM LAGER YAKABIDHI SH MILIONI 20 KWA AJILI YA MKUTANO MKUU WA YANGA

Mkurugenzi wa Uhusiano na Masuala ya Sheria (Director of Corporate and Legal Affairs) wa kampuni ya bia (TBL), Steve Kilindo (kulia), akikabidhi hundi ya shilingi milioni 20 kwa Katibu wa Yanga, Celestine Mwesiga. Fedha hizo zimetolewa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager ikiwa kwa ajili ya mkutano mkuu wa Yanga ikiwa ni sehemu ya udhamini wake kwa klabu hiyo. Wanaoshuhudia ni Jaji John Kkwawa, Mwenyekiti wa Kamati ya uchaguzi wa Yanga (mwenye miwani), na Kaimu Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Oscar Shelukindo. (Picha: Hisani ya Executive Solutions)

IKIWA ni sehemu ya udhamini wake kwa klabu ya Yanga, bia ya Kilimanjaro Premium Lager leo imekabidhi Sh. Milioni 20 kwa klabu hiyo kwa ajili ya mkutano mkuu utakaofanyika sambamba na uchaguzi wa uongozi mpya Julai 15,  mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe alisema: “Kilimanjaro Premium Lager inatambua wajibu wake na ina nia ya dhati kuendeleza soka. Kwa kwa kuzingatia hilo tungependa kuona maendeleo ya Yanga na ndio maana tunaiunga mkono klabu hii katika mkutano wake mkuu. Tunatambua kuwa hii ni klabu kubwa yenye historia kubwa na hivyo tunaamini kuwa inahitaji kuwa na uongozi bora, imara na madhubuti. 

“Tunatambua wajibu wetu kama wadhamini wakuu wa Yanga katika kutekeleza mkataba wetu, tutaendelea kushirikiana na kufanya kazi kwa pamoja ili kuhakikisha tunalipeleka soka la Tanzania kwenye kilele cha mafanikio”

Meneja wa Bia ya Kilimanjaro pia aliwasihi wajumbe wa mkutano mkuu kuhakikisha wanatimiza wajibu wao ipasavyo kwa kufanya uchaguzi wenye amani na kuchagua viongozi watakaofanya kazi kwa maslahi ya klabu.

No comments:

Post a Comment