Tuesday, July 24, 2012

WABUNGE WALIA NA MATUSI YA AKINA ‘KANGA MOJA NDEMBENDEMBE’, ‘KANGA MOKO LAKI SI PESA’ NA ‘KITU T’

Astaghafirullahi.... hii sasa noma. Uchezaji huu wa mnenguaji mmojawapo wa akina 'Kanga Moko' nd'o uliomchefua mbunge hadi akalalamika bungeni leo.
Mmmhhh... uchezaji gani huu jamani? Ndo mambo ya akina 'Khanga Moko Laki Si Pesa, Milioni Moja Paketi Money'
Tobaaa....! Namna hii tutasalimika kweli? Huyu naye ni memba wa walewale akina 'Kitu T' na 'Kanga Moko'
Uuuuwwwiiiii.....mwenzenu nafwa na kiuno hiki... haki ya nani siangalii tena!

Mtazame na huyu... nd'o walewale. Tatizo ni hiyo khanga yenyewe moja, ambayo unaambiwa imeloweshwa kidogo na kuwa ndembendembe! Kwanini wabunge wasihofie upotofu wa maadili?

Ohooo....! Hawa nao wamevaa vizuri katikati ya mwili, lakini chini ni khanga moja ndembendembe na bado wanajibinua kihasara hasara. Ni balaaa tupu!
Apo chachaaaa....! Huu wote ni uchokozi wa akina Khanga Moko  

Mama weeee.....! Hii si mitego jamani?

Wabunge wa viti maalum, Mhe. Tawhida wa Zanzibar na Mhe. Dk. Getrude Rwakatare wameitaka serikali kuchukua hatua za haraka kudhibiti vitendo vya uvaaji wa hovyo na unaokiuka maadili wa makundi ya unenguaji kama ya ‘Kanga Moja Ndembendembe Laki Si Pesa’.

Wabunge hao wameyasema hayo bungeni mjini Dodoma mchana huu wakati wakichangia hoja ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.

Awali, Mhe. Tawhida  alisema kwamba vivazi hivyo vya makundi kama ‘Khanga Moja Laki Si Pesa’ vinadhalilisha wanawake kwani wanenguaji wake huvaa khanga moja nyepesi inayoonyesha sehemu kubwa ya miili yao na pia uchezaji wao hujaa matusi ambayo hayapaswi kuachwa hivi hivi.

Wakati akielezea kilio chake kuhusiana na vikundi vya aina ya Khanga Moko, Mhe. Mchungaji Rwakatare alienda mbali zaidi kwa kufafanua kuwa wanenguaji hao (akina Khanga Moko) hulowesha khanga zao na kucheza kwa namna ambayo inakwenda kinyume na maadili.

Akaitaka serikali kuingilia kati na kuchukua hatua za kukomesha vikundi vya aina hiyo vinavyochangia sana katika kuharibu maadili.

2 comments: