Sunday, July 29, 2012

VAN PERSIE ATAKA MSHAHARA WA ROONEY ATUE MAN UTD

Robin van Persie

MUASI wa Arsenal, Robin van Persie anataka kuwa mshahara sawa na wa Wayne Rooney kama Manchester United wanataka ajiunge nao.

Gazeti la Daily Star Sunday limesema kuwa Van Persie atajiunga na Man United kama ataahidiwa mshahara mkubwa kama wa Rooney.

Nyota wa timu ya taifa ya England, Rooney ndiye mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa zaidi klabuni Man United ambao ni paundi 220,000 (sawa na Sh. milioni 537) kwa wiki na mshambuliaji wa Arsenal, RVP anataka mshahara kama huo.


No comments:

Post a Comment