Friday, July 20, 2012

UWANJA WA REAL MADRID SASA KUITWA 'FLY-EMIRATES-BERNABEU'


Simba na Yanga mpo? Tazama liuwanja la Santiago Bernabeu linavyoonekana kwa nje.

Hivi ndivyo 'liuwanja' la Santiago Bernabeu linavyoonekana sasa kwa juu.

'Liuwanja' la uwekli la Santiago Bernabeu linavyoonekana kwa ndani.

Hapa 'liuwanja' la Santiago Bernabeu linavyoonekana kwa ndani katika engo tofauti.

Liuwanja la Santiago Bernabeu linavyoonekana kwa ndani baada ya kujaa mashabiki.
MADRID, Hispania
Real Madrid imeripotiwa kuwa inafikiria kuupa jina jingine uwanja wake wa Santiago Bernabeu ikiwa ni sehemu ya makubaliano waliyofikia na mdhamini Emirates.

Kwa mujibu wa ABC, Real hawako tayari kutekeleza wazo la kuondosha kabisa jina la awali la uwanja ambalo ni la rais gwiji wa klabu hiyo. Hata hivyo, hawapingi jina hilo kutanguliwa na la kampuni inayowadhamini.

Kwa sababu hiyo, Emirates, ambayo hivi karibuni imeingia mkataba wa miaka mitano wa kudhamini jezi za Real, sasa inatoa ofa ya kuongeza euro milioni 53 katika kila msimu ili kubadili jina la kiwanja kimojawapo maarufu cha soka duniani na kuitwa 'Fly-Emirates-Bernabeu'.

Kadri ya hali ilivyo sasa, shirika hilo la ndege lenye maskani yake mjini Dubai, na ambalo hivi sasa lina haki za jina la uwanja wa Arsenal, litakuwa na haki ya kuona kuwa logo ya kampuni yake ikitumika katika jezi za Real Madrid kuanzia mwaka 2013 na kuendelea.

Uwanja wa Santiago Bernabeu ulizinduliwa mwaka 1947 na, kufuatia upanuzi wake mwaka 2011, sasa una uwezo wa kuchukua watazamaji 85,454.

No comments:

Post a Comment