Mbwana Samatta wa TP Mazembe (kulia) akifanya vitu vyake katika moja ya mechi za klabu yake. |
LUBUMBASHI, Kongo
MSHAMBULIAJI Emmanuel Clottey
alifunga mara mbili na kuisaidia Berekum Chelsea ya Ghana kuishikilia TP Mazembe
ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa sare ya mabao 2-2 katika mechi yao ya
Kundi B la Ligi ya Klabu Bingwa Afrika mjini Lubumbashi jana.
Clottey alifunga mara mbili
katika kipindi cha pili na kuongeza idadi ya mabao aliyofunga katika michuano
hiyo ya juu kwa ngazi ya klabu kufikia 11 wakati akiisaidia timu yake
kusawazisha baada ya kuwa nyuma kwa mabao mawili hadi kufikia mwisho wa kipindi
cha kwanza.
Matokeo hayo yameifanya klabu
hiyo kuendelea kuwa wawakilishi wazuri wa Ghana, ikiwa ni mechi yao ya pili
baada ya awali kushinda nyumbani kwao jijini Accra kwa mabao 3-2 dhidi ya
vigogo wa Misri, klabu ya Zamalek.
Wakihitaji ushindi ili
kujiongezea matumaini ya kufuzu kupitia kundi lao, TP Mazembe anayochezea
Mtanzania Mbwana Samatta ilianza kwa kasi, ikiwabana wageni kwenye eneo la nusu
ya uwanja wao. Walipata bao la utangulizi katika dakika ya 10 wakati nahodha
wao Tresor Mputu Mabi alipofunga kwa shuti la karibu na lango na kuibua shangwe
kwenye uwanja uliofurika mashabiki wa Frederic Kibassa Maliba.
Dakika chache baadaye, ‘besela’
liliwanyima bao Mazembe baada ya shuti kali la Mzambia Rainford Kalaba kuparaza
na kutoka nje.
Katika dakika ya 31, wenyeji
walipata goli la pili hatimaye kutokana na penati iliyopigwa na Mputu. Beki
Edward Kpodo alidaiwa kumkwatua Mputu ndani ya eneo la hatari. Kipa Sowah wa
Chelsea alipangua penati hiyo kabla Mputu kuwahi mpira huo na kufunga.
Berekum Chelsea walipewa penati
katika dakika ya 70 baada ya kipa wa Mazembe, Muteba Kidiaba kumuangusha
Clottey wakati alipobaki naye ndani ya eneo la 18. Clottey akafunga penati hiyo
Dakika sita kabla ya mechi
kumalizika, Clottey (24), aliye katika kiwango chake cha juu cha ufungaji,
alizima kelele za wenyeji wakati alipowatoka mabeki wawili wa Mazembe kabla ya
kupiga shuti la kubetua lililompita Kidiaba na kujaa wavuni.
No comments:
Post a Comment