Messi akikokota mpira mbele ya kocha Diego Maradona. |
Lionel Messi (kushoto) na Ronaldo wanavyoonekana katika mechi mojawapo ya La Liga kati ya Barcelona na Real Madrid. |
GWIJI wa Argentina, Diego Maradona amesema kuwa Straika Cristiano
Ronaldo wa Real Madrid kamwe hatafikia mafanikio ya Muargentina mwenzake Lionel
Messi wa klabu ya Barcelona.
Kuna mashabiki wengi wanaoamini kwamba Ronaldo alimfunika Messi
msimu uliopita licha ya kwamba Muargentina huyo (Messi) aliongoza katika ‘ligi’ ya upachikaji
mabao.
Lakini Maradona anasema: "Cristiano hatafikia hata siku
moja mafanikio ambayo tayari Messi ameshayapata, ni kweli ana mashuti mazuri
sana, lakini anahitaji kuwa na vitu vingine zaidi ya mashuti.
"Sitamzungumzia Messi kwa mabaya hata siku moja kwa sababu
namjua… Messi anafunga magoli na kushangilia, Cristiano anafunga magoli na
kusimama kama vile mtu anayeuza shampoo. Hiyo nd’o tofauti yao."
No comments:
Post a Comment