|
Lahaulaa...! Eti hapa madada walioshinda wanapongezana. |
|
Jennifer Kessy (kushoto) akijaribu kuzuia mpira unaopigwa na Kerri Walsh. Timu ya Kessy ilishinda 2-0. |
|
Holly McPeak na mwenzake Jennifer Kessy wakirudisha mpira uliopigwa na Kerri Walsh na mwenzake Misty May-Treanor wakati wa kuwania taji la AVP Hermosa Beach Open kwenye fukwe za Hermosa. |
|
Nyota wa Marekani, Kerri Walsh na Misty May-Treanor wakipongezana. |
|
Misty May-Treanor na Kerri Walsh (kushoto) wakikumbatiana kupeana moyo kabla ya kuwavaa Larissa Franca na Ana Paula Conelly wa Brazil |
|
Hee... kumbe hata Rihanna yumo. Hapa anajiachia na mpira wa wavu kwenye fukwe za Ugiriki. |
|
Tobaaa...! Sasa mchezo gani huu? Mcheki Rihanna alivyojibinua kiuchokozi baada ya kunogewa na mpira wa wavu wa ufukweni wakati akiwa mapumzikoni Ugiriki. |
LONDON, England
BIKINI za Kibrazili ni ruksa kutumika katika
michuano ya mpira wa wavu ya ufukweni wakati wa michezo ya Olimpiki
itakayofanyika jijini London kuanzia wiki ijayo.
Imeelezwa na waandaaji jijini London leo
kuwa vivazi hivyo vya wachezaji vimeruhusiwa kwa vile ni miongoni mwa vivutio
vikubwa kwa watazamaji.
Mchezo huo ulianza kujumuishwa rasmi kwa
mara ya kwanza katika michezo ya Olimpiki kwenye fukwe za California mwaka
1996, lakini tangu wakati huo umekuwa ukipingwa na baadhi ya wahafidhina wanaohoji
kitendo cha kuruhusu mchezo unaowaacha wanawake wakiwa na viguo vya kuogelea kuwemo
katika ratiba ya Olimpiki.
Nchi za Marekani, Brazil na Australia ndizo
hutawala zaidi katika mchezo wa mpira wa wavu wa ufukweni na ndio pekee hadi
sasa zilizowahi kutwaa medali za dhahabu katika michuano ya Olimpiki huku
wakali waliowahi kutwaa dhahabu mara mbili wakiwa ni pamoja na Wamarekani Misty
May-Treanor, 34 na Kerri Walsh, 33.
No comments:
Post a Comment