Tuesday, July 24, 2012

TIM CAHILL AJIUNGA NA THIERRY HENRY

Tim Cahill

EVERTON imeafikiana bei na klabu ya New York Red Bulls kwa ajili ya uhamisho wa kiungo wa Australia, Tim Cahill kwenda kwenye timu hiyo ya Ligi Kuu ya Marekani anayoichezea mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Thierry Henry.

"Tim atahamia Red Bulls kwa ada iliyofichwa, kutegemea maafikiano binafsi ya mchezaji na kama atafuzu vipimo vya afya. Atasafiri kwenda Marekani katika siku chache zijazo," Everton ilisema katika tovuti yao (www.evertonfc.com).

Vyombo vya habari wa Uingereza vimeripoti kuwa ada ya uhamisho huo ni  dola milioni 1.55.

Kiungo huyo wa ushambuliaji mwenye umri wa miaka 32 alifunga magoli 68 katika mechi 278 alizoichezea Everton baada ya kujiunga na klabu hiyo akitokea Millwall mwaka 2004.

Pia amefunga magoli 24 katika mechi 55 za timu yake ya taifa ya Australia na amecheza fainali mbili za Kombe la Dunia nchini Ujerumani na Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment