Saturday, July 21, 2012

THIAGO SILVA: LUCAS ATATISHA MAN U KAMA RONALDO, NANI


Lucas Moura
Thiago Silva
PARIS, Ufaransa
BEKI mpya wa PSG, Thiago Silva hashangazwi kuona kuwa Manchester United wanahaha kumsajili mchezaji nyota wa klabu ya Sao Paulo ya Brazil, Lucas Moura.

Silva ambaye ni nahodha wa timu ya taifa ya Brazil itakayoshiriki michuano inayoanza wiki ijayo ya Olimpiki jijini London na hivyo kuwa karibu na Moura kwenye kikosi chao cha taifa, amemuelezea Moura kuwa ni mchezaji mwenye kipaji cha hali ya juu.

"Naona kuna kila dalili kwa Lucas kucheza katika Ligi Kuu ya England," alisema Silva.
"Licha ya kuwa ni mfupi, yeye ni ngangari na pia ana nguvu za kutosha. Ni vigumu sana kumzuia.

"Na kwa kawaida katika klabu ya Manchester, wanacheza na mawinga wawili -- alitamba Cristiano Ronaldo na sasa ni zamu ya Nani. Lucas ana sifa zote walizo nazo wakali hawa (Ronaldo na Nani)."

No comments:

Post a Comment