Straika Robin Van Persie |
MANCHESTER
HATIMAYE klabu mahasimu za Manchester
City na Manchester United zimetuma maombi rasmi ya ya kumtwaa straika nyota aliyekataa
kusaini mkataba wa Arsenal, Robin van Persie.
Gazeti la The Sun limesema
leo kuwa Man City wametuma ofa ya paundi za England milioni 15 kwa Arsenal jana
(bilioni 36) huku pia kocha wa Man U, Alex Ferguson akithibitisha kutuma ofa ya
kumtwaa kwa paundi za England milioni 13 (Sh. Bilioni 32).
Hata hivyo, Arsenal
wamekaririwa wakisema kuwa hawako tayari kumuachia nahodha wao huyo aliyeibuka mfungaji
bora wa Ligi Kuu ya England msimu uliopita kwa dau lisilofikia walau paundi za
England milioni 20 (Sh. Bilioni 50)
Juventus pia wamejitosa
katika vita ya kumuwania na tayari wameshatoa ofa ya kumtwaa kwa paundi za
England milioni 8 (Sh. Bilioni 20).
Jana, Arsenal walisema kuwa
wako radhi kumuachia ikiwa watapewa ofa sahihi itakayofikia dau wanalotaka.
No comments:
Post a Comment