Thursday, July 26, 2012

NYOTA WAWILI WAPYA BARCA NJE MIEZI MITATU, SITA

Kiungo mpya wa Barcelona, Edgar le akiwa na magongo baada ya kuumia.

BARCELONA imekiri kwamba kiungo wao mpya waliyemsajili wiki iliyopita kutoka  Sporting Lisbon, Edgar Ie, atakuwa nje ya uwanja kwa miezi mitatu.

Klabu hiyo imesema kuwa Edgar Ie atakuwa nje ya uwanja kutokana na kufanyiwa upasuaji wa mguu.

Edgar alitua Barcelona wiki iliyopita pamoja na Agostinho Ca wote wakitokea Sporting kwa mkataba wa miaka minne kila mmoja.

Aidha, kiungo mwingine wa Barca, Marc Muniesa huenda akakaa nje ya uwanja kwa miezi sita baada ya kuumia goti katika mechi ya kirafiki waliyoshinda 2-1 dhidi ya Hamburg juzi.

Mchezaji huyo wa timu ya taifa ya Hispania ya vijana wa umri chini ya miaka 21, alipata majeraha hayo mwanzoni mwa kipindi cha pili cha mechi hiyo na vipimo vimethibitisha kwamba ameumia kwa ndani goti lake la kulia.

Itaamuliwa ndani ya siku chache ni lini kiungo huyo mwenye umri wa miaka 20 ataenda kufanyiwa upasuaji lakini anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa miezi sita, Barca ilitangaza katika tovuti yao.

No comments:

Post a Comment