Thursday, July 26, 2012

DANI ALVES HAUZWI - VILANOVA

Dani Alves

KOCHA wa Barcelona, Tito Vilanova amesisitiza kwamba bado anamtegemea beki wa kulia Daniel Alves.

Beki huyo aliishangaza menejimenti wiki iliyopita kwa kudai kwamba "anakosa sapoti" wakati uvumi kwamba atauzwa ukiwa juu.

"Hatujawahi kufikiria kumpoteza Alves," alisisitiza Vilanova.

"Ilikuwa ni juu ya mjadala ndani ya klabu.

"Yeye ndiye beki wa kulia bora zaidi duniani, mmoja wa wachezaji bora kabisa waliopata kusajiliwa na Barcelona katika miaka ya karibuni na mmoja wa wachezaji ambao ni muhimu zaidi katika kuchezesha timu yetu."

No comments:

Post a Comment