Mv Kalama |
Mv Kalama inavyoonekana kabla ya kupigwa stop kubeba abiria na Serikali ya Zanzibar leo |
Mv Skagit inavyoonekana baada ya kupinduka chini juu na baadhi ya abiria wake wakisubiri kuokolewa kabla ya kuzama yote baharini. |
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Balozi Seif Iddi |
Boti hiyo, ambayo pia inamilikiwa na kampuni
ya Seagull Transport Sea Company Limited kama ilivyokuwa Mv Skagit, sasa
haitaruhusiwa kujihusisha kabisa na biashara ya usafirishaji wa abiria katika visiwa hivyo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar,
Balozi Seif Iddi, alithibitisha juu ya uamuzi huo wa serikali leo wakati
akipokea mchango wa Sh. milioni 10 kwa ajili ya wahanga wa ajali ya kuzama kwa Mv Skagit kutoka kwa
Shirika la Mfuko wa Ustawi wa Jamii (NSSF) na kukabidhiwa na mkurugenzi wa mfuko huo, Dk.
Ramadhani Dau.
Jana, serikali ya Zanzibar iliunda tume ya kuchunguza sakata la kuzama kwa Mv Skagit katika eneo la Chumbe wakati ikitokea Dar es Salaam kwenda Zanzibar huku ikiwa na watu wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 340.
Tayari aliyekuwa waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Zanzibar, Hamad Masoud Hamad ametangaza kujiuzuku kutokana na tukio hilo ambalo limeibua maswali mengi kwani taarifa zilizopo, na ambazo sasa zimethibitishwa kutokana na uamuzi uliotangazwa na Balozi Iddi, zinadai kwamba boti hizo (iliyozama ya Skagit na Mv Kalama) ziliengenezwa kwa ajili ya kufanya kazi kama vivuko tu, zikitakiwa kutembea umbali mfupi.
No comments:
Post a Comment