Sunday, July 29, 2012

NEYMAR AFANYA MAKUBWA OLD TRAFFORD

Mshambuliaji wa Brazil, Alexandre Pato (katikati) akishangilia goli lake dhidi ya kipa wa Belarus, Aleksandr Gutor (kulia) aliyelala chini huku Igor Kuzmenok akishuhudia wakati wa mechi yao ya Kundi C la michuano ya soka ya Olimpiki ya London 2012 kwenye Uwanja wa Old Trafford mjini Manchester leo Julai 29, 2012. Krosi ya goli hilo ilitolewa na Neymar, ambaye pia alifunga goli moja kwa fri-kiki ya hatari iliyokwenda moja kwa moja wavuni. Brazil ilishinda 3-1. Picha: REUTERS

Mshambuliaji wa Brazil, Neymar (kulia) akiwania mpira dhidi ya mchezaji wa Belarus, Renan Bardini Bressan wakati wa mechi yao ya Kundi C la michuano ya Olimpiki ya London 2012 kwenye Uwanja wa Old Trafford mjini Manchester Julai 29, 2012. Picha: REUTERS

No comments:

Post a Comment