Jose Mourinho akishangilia baada ya kutwaa taji la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya wakati akiifundisha Inter Milan ya Italia. |
LISBON, Ureno
KOCHA wa Real Madrid, Jose Mourinho atapokea
tuzo ya Fernando Soromenho Ijumaa ambayo hutolewa na Chama cha Waandishi wa Habari za
Michezo Ureno (CNID) kutokana na mafanikio yake katika mchezo wa soka.
Kocha huyo mwenye miaka 49, atakabidhiwa tuzo
hiyo kwenye hoteli ya Pestana Palace mjini Lisbon, na baada ya
hapo atazungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari.
Hiyo ni tuzo inayopewa heshima ya
juu zaidi kutoka CNID, ambayo ilianzishwa mwaka 1967.
Mourinho, aliyeanza kazi ya ukocha
mwaka 2000 katika klabu ya Benfica, aliisaidia Porto kutwaa taji moja la Kombe
la UEFA na kombe jingine la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya katika kipindi cha miaka
miwili ya kuiongoza klabu hiyo.
Akaendeleza moto wake kwa kutwaa
mataji kadhaa baada ya kuhamia Chelsea na Inter Milan kabla ya kutua Real
Madrid wakati wa usajili wa majira ya kiangazi mwaka 2010. Hadi sasa, tayari
ameshaipa Real Madrid Kombe la Mfalme (Copa del Rey) na jubingwa wa La Liga,
Ligi Kuu ya Hispania.
No comments:
Post a Comment