Tuesday, July 24, 2012

BAHANUZI APITWA MAGOLI KAGAME

Said Bahanuzi akishangilia moja ya mabao yake dhidi ya Wau Salaam ya Sudani Kusini kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumanne Julai 17, 2012. Bahanuzi alifunga magoli mawili, Yanga ilishinda 7-1. Picha: Globalpublishers.info

MSHAMBULIAJI wa Yanga, Said Bahanuzi amepitwa kwa goli moja na Taddy Etikiema wa Vita Club ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo baada Etikiema kuifungia timu yake goli la kuongoza katika dakika ya 7 ya mechi yao ya robo fainali ya Kombe la Kagame waliyoshinda 2-1 dhidi ya Atletico ya Burundi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam dhidi ya Atletico ya Burundi.

Vita sasa itacheza nusu fainali dhidi ya mshindi wa mechi inayoanza hivi punde baina ya Simba na Azam FC zote za Dar es Salaam.

Taddy alifunga goli hilo akitumia makosa ya beki kujichanganya wakati akimrudishia mpira kipa wake.

Etikiema sasa amefikisha magoli 6 katika mechi nne na kumuacha Bahanuzi akiwa na magoli 5. 

Bahanuzi alifunga goli lake la tano kwa kichwa jana kufuatia krosi ya beki mpya wa kulia Juma Abdul katika dakika ya kwanza ya kipindi cha pili na kuisawazishia timu yake ya Yanga iliyoenda mapumziko ikiwa nyuma kwa bao 1-0 dhidi ya mabingwa wa Zanzibar, Mafunzo. 


Goli hilo la Bahanuzi liliilazimisha mechi hiyo kuamuliwa kwa kupigiana penalti baada ya dakika dakika 90 kumalizika matokeo yakiwa 1-1. Yanga walishinda kwa penalti 5-3 na kutinga nusu fainali ambapo sasa watawakabili APR ya Rwanda keshokutwa.


Vikosi katika mechi inayotarajiwa kuanza punde ni; Simba: Juma Kaseja, Haruna Shamte, Shomari Kapombe, Lino Masombo, Juma Nyosso, Mussa Mude, Jonas Mkude, Mwinyi Kazimoto, Haruna Moshi 'Boban', Felix Sunzu na Uhuru Selemani.

Azam: Deogratius Munishi 'Dida', Ibrahim Shikanda, Erasto Nyoni, Said Morad, Aggrey Morris, Kipre Bolou, Kipre Tchetche, Salum Aboubakar, John Bocco 'Adebayor', Ibrahim Mwaipopo na Khamis Mcha.  



No comments:

Post a Comment