Wananchi wakiendelea na zoezi la uopoaji maiti za ajali ya kuzama kwa Mv Skagit. |
Maiti zaidi wakiteremshwa baada ya kuopolewa baharini. |
Miili mingine 21 ya watu waliozama na
boti ya Mv Skagit iliyokuwa ikisafiri kutoka jijini Dar es Salaam kuelekea
Zanzibar imepatikana leo na hivyo kuongeza idadi ya maiti wote waliopatikana
kufikia 98.
Taarifa zilizothibitishwa na Polisi Zanzibar
jioni hii zimeeleza kuwa miili hiyo imepatikana katika maeneo mbalimbali,
yakiwamo ya Chumbe kulikotokea ajali hiyo, Pume na Punguja.
Jeshi hilo limesema kuwa miongoni mwa
miili iliyopatikana, umo wa mgeni mmoja kutoka Uholanzi na kwamba.
Licha ya awali kutangazwa na Serikali juu ya kusitishwa rasmi kwa zoezi la kutafuta miili zaidi, bado juhudi zimekuwa zikiendelea kufanywa na serikali kwa kushirikiana na wananchi katika kusaka miili ya watu waliokufa kutokana na ajali hiyo.
Licha ya awali kutangazwa na Serikali juu ya kusitishwa rasmi kwa zoezi la kutafuta miili zaidi, bado juhudi zimekuwa zikiendelea kufanywa na serikali kwa kushirikiana na wananchi katika kusaka miili ya watu waliokufa kutokana na ajali hiyo.
Wakati ikizama katika eneo la Chumbe,
boti hiyo ilikuwa na watu zaidi ya 340. Inahofiwa kuwa baadhi ya miili ya
waliokufa bado imenasia ndani ya boti hiyo ambayo imezama chini kabisa mwa kina
kirefu cha bahari kinachokadiriwa kuwa ni cha zaidi ya mita 60.
Boti ya Mv Skagit ilikumbwa na ajali hiyo Julai 19 wakati
ikiwa katika eneo la Chumbe. Ilidaiwa kwamba awali ilipigwa na
dhoruba kali mishale ya saa 7:00 mchana, ikapinduka na kisha boti hiyo ndipo ikazama yote
baharini.
No comments:
Post a Comment