Tuesday, July 24, 2012

RAIS WA GHANA ATTA MILLS AFARIKI GHAFLA LEO

ALIINGIA MADARAKANI AKITOKEA UPINZANI 2009

Hayati Atta Mills enzi za uhai wake.

ACCRA, Ghana

Rais wa Ghana, John Atta Mills, aliyekuwa akisumbuliwa na maradhi ya kansa ya koo, amefariki dunia katika jiji kuu la nchi hiyo, Accra.


Taarifa kutoka katika ofisi yake yake zilieleza kuwa rais huyo mwenye miaka 68 alikufa saa chache tu baada ya kuzidiwa, lakini hakukuwa na maelezo zaidi.


"Kwa huzuni kubwa... tunatangaza juu ya kifo cha ghafla na kisichotarajiwa cha rais wa Jamhuri ya Ghana," taarifa hiyo ilisema.


Atta Mills ameliongoza taifa hilo la magharibi mwa Afrika tangu mwaka 2009 wakati chama chake kilichokuwa cha upinzani kiliposhinda katika uchaguzi mkuu wan chi hiyo.


Msaidizi wa rais amesema kwamba Atta Mills alilalamika kusumbuliwa na maumivu jana jioni na akafa leo mchana, shirika la habari la Reuters liliripoti.


Alirejea Ghana baada ya kutoka Marekani alikokwenda kuchunguzwa afya yake.

No comments:

Post a Comment