Friday, July 20, 2012

MAN U SASA WAMTOLEA MACHO NURI SAHIN WA REAL MADRID


Nuri Sahin
MANCHESTER United sasa wameelekeza macho yao kwa kiungo wa Real Madrid, Nuri Sahin baada ya kuona wakikatishwa tama na mpango wao wa kumnasa Mbrazili Lucas Moura.

Straika (kupitia mtandao wa Goal.com), inatambua kwamba Man U wanasaka kiungo mwingine badala ya chipukizi Moura wa  Sao Paulo, ambaye bei ya kumnunulia waliyotajiwa na klabu yake ni euro milioni 38.3, na wamegusia kwamba Sahin ni ‘kifaa’ watakachokiata kwa bei poa baada ya nyota huyo kutambua ugumu wa kupata namba katika kikosi cha mabingwa wa La Liga, Real Madrid.

Kiungo huyo wa kimataifa wa Uturuki  amekuwa ni mchezaji wa ziada katika kikosi cha Real tangu alipotua akitokea Borussia Dortmund msimu uliopita na kuandamwa na majeraha na kucheza kwa kiwango cha chini.

Jose Mourinho anaweza kumhakikishia Sahin nafasi ya kutosha ya kucheza katika mechi zao za maandalizi ya msimu ili kuona kama atafaa kuwemo katika kikosi cha vigogo hao wa La Liga, lakini ni wazi kwamba Real watakuwa tayari kusikiliza ofa kutoka kwa Man U.

Bayern Munich na Galatasaray zimekuwa pia zikihusishwa na usajili wa Sahin katika wiki za hivi karibuni. Tottenham pia walituma ombi la kumtaka ili atumike kubadilishana naye na kiungo wao Luka Modric anayetakiwa sana na Real Madrid, lakini ‘wakala za uso’ baada ya Sahin mwenye miaka 23 kukataa kutumika kama chambo.

Sahin amesisitiza kuwa anataka kubaki Real Madrid msimu ujao ili apiganie namba katika kikosi cha kwanza, akisema: "Nina usongo wa kupata mafanikio hapa na ninataka kuthibitisha thamani yangu kwa Real Madrid. Nina ndoto za kutimiza katika klabu hii."

No comments:

Post a Comment