Rio Ferdinand |
Ferguson akiingia na timu yake uwanjani wiki iliyopita katika mechi za maandalizi ya msimu nchini Afrika Kusini. |
LONDON, England
KOCHA wa Manchester United, Sir Alex Ferguson amefichua kuwa
hatarajii kumuona tena beki wake Rio Ferdinand akiichezea tena timu ya taifa ya
England.
Licha ya kuwahi kuichezea timu ya taifa hilo mara 81, beki
huyo wa kati aliachwa katika kikosi cha awali
cha nchi yake kilichoshiriki fainali za Euro 2012, na baadaye akatoswa tena licha
ya beki aliyetrajiwa kutwaa mikoba yake, Gary Cahill kujiondoa kutokana na
majeraha.
Kocha Roy Hodgson wa timu taifa ya England alisisitiza kwamba
alichagua kikosi chake kwa kuzingatia sababu za kiufundi lakini Ferdinand alielezea
kutofurahishwa kwake na hatua hiyo kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter,
akigusia uvumi kwamba ameachwa kwa sababu ya mtafaruku uliopo baina ya John
Terry na mdogo wake, Anton Ferdinand.
"Sidhani (kama Ferdinand ataichezea tena timu ya taifa
ya England). Sioni uwezekano huo. Hilo halipo katika mipango yake,"
Ferguson aliwaambia waandishi wa habari.
"Sasa ana miaka 33 na anataka kuwa fiti ili aitumikie klabu yetu.
Ukiwa kama beki wa kati, ukijitunza vizuri unaweza kucheza hadi kufikia miaka 37.
"Rio alicheza vizuri kwetu msimu uliopita. Pengine anaichezea
kwa kiwango cha juu timu yetu na kwa muda mrefu kwa sababu alikuwa akicheza
kila mara. Misimu miwili iliyopita amekuwa akicheza kila wiki, anakuwa nje kwa
wiki tatu, halafu anarudi tena.
"Yeye na Jonny Evans walionyesha kiwango kizuri wakiwa pamoja
na kuendelea hivyo kuanzia Desemba hadi Februari na Machi."
Wakati nahodha wa klabu hiyo, Nemanja Vidic akijiandaa
kurejea kikosini baada ya kutumia muda mwingi wa msimu uliopita akiwa nje
kutokana na jeraha la goti, Ferdinand anakabiliwa na ushindani mkali wa kuwanian
namba katika kikosi cha kwanza, tofauti na msimu uliopita.
No comments:
Post a Comment