Tuesday, July 17, 2012

LUKAKU ACHOSHWA BENCHI CHELSEA, KUTIMKIA FULHAM

Romelu Lukaku

 
LONDON, Chelsea
STRAIKA wa Chelsea Romelu Lukaku yuko katika hatua za mwisho kusajiliwa kwa mkopo na klabu ya Fulham, imefahamika.

Mahasimu hao wa wa Jiji la London wako katika hatua nzuri ya mazungumzo kuhusiana na mpango huo ambao utamfanya Lukaku achepukie upande mwingine wa mji kwa mkataba mrefu wa mkopo.

Martin Jol ameruhusu uhamisho wa yosso huyo wa Mbelgiji baada ya Chelsea kusema wazi kwamba ilikuwa ikiangalia uwezekano wa kuwatema, ama kwa kuwauza kwa mkopo au kuwauza jumla baadhi ya wachezaji wake wa kikosi cha kwanza.

Chelsea hawana kikwazo katika kumruhusu Lukaku, 19, kwenda Fulham ikiwa atahakikishiwa nafasi zaidi za kucheza kulinganisha na ile aliyo naso sasa Stamford Bridge.
Lukaku amezungumzia kutofurahishwa kwake na hali ya kutopewa nafasi ya kutosha ya kucheza katika kikosi cha kwanza tangu asajiliwe na Chelsea mwanzoni mwa msimu uliopita kwa dau la  paundi za England milioni 18 akitokea Anderlecht.

Alisema kuwa “ameksirishwa sana” kuona kuwa ameanzishwa katika mechi moja tu ya Ligi Kuu ya England na kudai kwamba hakutendewa haki na kocha wa zamani wa Chelsea, Andre Villas-Boas.

Licha ya kuondoka kwa Didier Drogba na Salomon Kalou katika kipindi hiki cha usajili wa majira  ya kiangazi na Nicolas Anelka aliyeondoka Januari, Lukaku bado hana uhakika wa kucheza mbele ya mastraika  Fernando Torres na Daniel Sturridge.

Chelsea na Fulham wameshakubaliana katika mambo ya msingi ya uhamishjo wake wa mkopo, ambao unaweza kufanana kwa kiasi kikubwa na wa Gael Kakuta katika mzunguko wa pili wa msimu wa 2010-11, wakati mshahara wa yosso huyo Mfaransa ulipochangiwa kwa kiwango sawa na klabu hizo mbili.   

Kama uhamisho huo utakamilishwa, Lukaku atakuwa ni mshambuliaji wa tatu kusajiliwa na Fulham katika dirisha hili la usajili.

Klabu hiyo ya magharibi mwa London tayari imeshawasajili Mladen Petric na Hugo Rodallega waliokuwa huru, kutoka katika klabu za Hamburg na Wigan Athletic, lakini ikamuuza Andy Johnson kwa QPR na pia kushindwa katika mchuano wake dhidi ya Reading kumuwania Mrusi Pavel Pogrebnyak, nyota wao waliyemtwaa kwa mkopo msimu uliopita.

No comments:

Post a Comment