Monday, July 16, 2012

LUKA MODRIC AKATAA MANOTI KIBAO TOTTENHAM KUFUATA MSHAHARA KIDUCHU REAL MADRID

Luka Modric

Mwenyekiti wa klabu ya Tottenham inayoshiriki Ligi Kuu ya England, Daniel Levy amestushwa na uamuzi wa kiungo wao Luka Modric aliyekataa kusaini mkataba mpya uliomboreshea mshahara wake mara mbili ili aichezee Real Madrid inayoshikilia ubingwa wa La Liga, Ligi Kuu ya Hispania.

Modric, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Croatian, amekataa kusaini mkataba mpya wa kumbakiza Tottenham, ambao ungemfanya awe mchezaji anayelipwa fedha nyingi zaidi katika historia ya klabu hiyo ya jiji la London.

Real wamempa Modric ofa ya kumlipa mshahara wa Euro milioni 4.5 kwa mwaka (Sh. bilioni 8.5), wakati mkataba waliomuandalia Tottenham ili abaki unamhakikishia mshahara mnono wa Euro milioni 5.4 kwa mwaka (Sh. bilioni 10).

Kwa kumaliza kileleni mwa La Liga msimu uliopita, Real Madrid watashiriki Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya wakati Tottenham watashiriki michuano midogo ya Ligi ya Europa baada ya kumaliza katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England, lakini wakipokwa nafasi ya kushiriki klabu bingwa Ulaya kwavile Chelsea iliyomaliza nje ya ‘top 4’ ilitwaa ubingwa wa Ulaya na hivyo imejihakikishia nafasi ya kutetea taji hilo.


No comments:

Post a Comment