JOHANNESBURG, Afrika Kusini
Ratiba ya raundi ya mwisho ya kuwania kufuzu kwa fainali za zijazo za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2013) imetolewa usiku huu ambapo kutakuwa na mechi za nyumbani na ugenini na washindi wa jumla katika kila mechi ndio watakaoungana na wenyeji Afrika Kusini katika kinyang’anyiro kitakachoanza Januari mwakani.
Vigogo Ivory Coast na Senegal ambao waliambulia patupu katika fainali zilizopita (AFCON 2012) licha ya kutabiriwa awali kuwa ndio watakaobeba taji hilo, wamepangwa pamoja huku mabingwa watetezi, Zambia wakikumbana na akina Emmanuel Okwi wa timu ya taifa ya Uganda ‘The Cranes’.
Mechi hizo zimepangwa kama ifuatavyo:
Mali v Botswana
Zimbabwe v Angola
Ghana v Malawi
Liberia v Nigeria
Zambia v Uganda
Cape Verde v Cameroon
Mozambique v Morocco
Sierra Leone v Tunisia
Guinea v Niger
Sudan v Ethiopia
Libya v Algeria
Ivory Coast v Senegal
DR Congo v Eq. Guinea
Gabon v Togo
Jamhuri ya Afrika ya Kati v Burkina Faso
Mechi za awali zitaanza kuchezwa kati ya Septemba 7-9 huku marudiano yakiwa kati ya Oktoba 12-14.
No comments:
Post a Comment