Thursday, July 5, 2012

MSOME KOCHA MPYA YANGA ALICHOIAMBIA STRAIKA

Kocha mpya wa Yanga, Tom Saintfeit (katikati) akiwa na Katibu Mkuu wa Yanga, Selestine Mwesigwa (kulia) na mgombea wa kiti cha Ujumbe wa Kamati ya Utendaji wa Yanga, Peter Haule (kushoto) wakati wa mazoezi ya Yanga leo asubuhi kwenye Uwanja wa Bora, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Picha: Sanula Athanas

Kocha mpya wa Yanga, Tom Saintfeit (katikati) akiwa na mmoja wa wafadhili wa Yanga, Abdala Bin Kleb (kushoto) na mgombea wa kiti cha Ujumbe wa Kamati ya Utendaji wa Yanga, Peter Haule (kulia) wakati wa mazoezi ya Yanga leo asubuhi kwenye Uwanja wa Bora, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Picha: Sanula Athanas

Mashabiki wakiwania kuingia kushuhudia mazoezi ya Yanga yaliyohudhuriwa kwa mara ya kwanza na kocha wao mpya Tom Saintfeit kwenye Uwanja wa Bora, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Picha: Sanula Athanas


Ngoja ninukuu majina ya wanaojua... kocha mpya wa Yanga, Tom Saintfeit (katikati) akichukua dondoo wakati wa mazoezi ya Yanga leo asubuhi kwenye Uwanja wa Bora, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Picha: Sanula Athanas

Kocha msaidizi wa Yanga, Fred Felix Minziro 'Majeshi' (kushoto) akiiongoza timu yake wakati wa mazoezi ya Yanga leo asubuhi kwenye Uwanja wa Bora, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Picha: Sanula Athanas

Nawanukuu wanaojua wawe kikosi cha kwanza... kocha mpya Tom akifanya mambo yake.

Tumepigwa 5-1 dah! Kweli timu kubwa ni kubwa tu. Wachezaji wa timu ya mchangani ya Shein Rangers ya Manzese wakipumzika wakati wa mechi yao ya kirafiki dhidi ya Yanga leo asubuhi kwenye Uwanja wa Bora, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Walilala 5-1. Picha: Sanula Athanas

Niyonzima, Shamte, Yondani, Taita.... tunapasha tu. Mambo ya leo hayo wakati wa mazoezi yao

Sisi tunaogopa 'fri-kiki' za kubutuana machoni.... Wachezaji wa Shein Rangers wakiweka ukuta wakati Rashid Gumbo akipiga 'fri-kiki' iliyokwenda wavuni baada ya kugonga nguzo. Picha: Sanula Athanas
Na Sanula Athanas
KOCHA mpya wa Yanga, Mbelgiji Tom Saintfiet amesema kwa sasa hauangalii upinzani ulipo kati ya klabu yake na klabu ya Simba kwa sababu ana jukumu la kuhakikisha anatetea Kombe la Kagame.

Kocha huyo aliyasema hayo leo asubuhi wakati wa mazoezi ya timu yake kwenye uwanja wa Bora, Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Saintfiet alisema anaelewa vizuri upinzani mkubwa uliopo kati ya klabu hizo nchini lakini aliweka wazi kuwa hayuko tayari kuifundisha Yanga kwa kuangalia mtindo ama mwenendo wa mahasimu wao, Simba.

“Nazijua vizuri sana Yanga na Simba na mambo yote yanayozihusu klabu hizi, lakini nimekuja kuing’arisha Yanga. Nimekuja kuinoa Yanga na jukumu kubwa nililonalo kwa sasa ni kuhakikisha inanyakua Kombe la Kagame,” alisema Saintfiet.

“Nimeiangalia timu yangu kwenye mazoezi, ina wachezaji wazuri. Nilipoambiwa wameshafanya usajili niliingiwa na hofu labda wamesajili wachezaji dhaifu lakini nimeona kuna wachezaji wazuri sana.” 

Kocha huyo ameeleza pia kufurahishwa na ukarimu wa Watanzania kwa mapokezi ambayo walimfanyia kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana.

No comments:

Post a Comment